Friday, July 26, 2013

Eti staa huyu wa Nollywood kasema hajakutana na mwanaume kimwili kwa miaka 10 sasa.


Kwenye zile stori za umbea kwa sasa huko Nigeria hii ni moja kati ya kubwa zake…

Mastaa wa kiwanda cha burudani mahali popote pale iwe ni Marekani au hapa nyumbani bongo wamekuwa na kawaida ya kujaribu kuhakikisha wanatafuta njia mbalimbali za ku-make headlines ambazo zitawafanya waweze kuendelea kuwa maarufu au kujipa promo kwa lengo flani.

Star wa Movie za Naija, Genevieve Nnaji ametoa kauli ambayo inaweza ikawa kali ya mwaka baada ya kuanika wazi kabisa siri zake za ndani za ishu za mapenzi yani.

Anakwambia hajawahi kufanya mapenzi kwa muda wa miaka kumi sasa hivi, amekuwa single kwa muda mrefu na kuna kipindi aliamua kuwekeza mawazo yake kwenye career au kazi yake ambayo ni kutengeneza filamu na ndio maana amekaa muda wote huo bila kufanya mapenzi.
Watu wengi watashangazwa na kauli hii kwa kuwa miaka si mingi staa huyu alikuwa akidaiwa ku-date na mwimbaji D’Banj ambapo anasema wakati anaingia kwenye uhusiano na mwimbaji huyo, D alisisitiza kuwa uhusiano huo sio wa muda mrefu na ndio maana wameachana.

Genevieve amewachanganya mashabiki wake kwa kauli nyingine yenye utata akizungumzia uhusiano wake na D’Banj ambapo alisema kuwa msanii huyo ana ‘uume’ mdogo, aliuona vipi wakati anadai hajafanya mapenzi kwa miaka kumi? swali gumu hilo…

No comments:

Post a Comment