Thursday, February 21, 2013

TAIFA STARS WAKABIDHIWA BASI LAO LA MIL.200 NA KILIMANJARO

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampauni ya Bia Tanzania (TBL) Robin Goetzsche (wa tatu kushoto) akikabidhi funguo kama ishara ya kukabidhi basi la Taifa Stars kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, Leodgar Tenga (wan ne kushoto) wakati Kilimanjaro Premium Lager ilipokabidhii basi hilo jana makao makuu ya TBL Jijini Dar es Salaam. Wengine kutoka kushoto ni Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kaviske, Mkurugenzi wa Masoko wa TBL Kushilla Thomas, Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen, Mchezaji wa Taifa Stars aliyewawakilisha wenzake, Erasto Nyoni, Katibu Mkuu wa TFF Angetile Osiah, Ofisa Mwandamizi wa Baraza la Michezo Tanzania, Chalukulu John na Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF Sunday Kayuni. (Picha na mpiga picha wetu).
Kocha wa Timu ya Taifa Kim Poulsen akishuka kutoka kwenye basi jipya la Taifa Stars lililolabidhiwa na Kilimanjaro Premium Lager.
Pichani juu na chini ni Washangiliaji mbalimbali wa Taifa Stars wakati Kilimanjaro Premium Lager ilipokabidhi basi jipya kwa Taifa Starsaifa katika makao makuu ya TBL Ilala jana.
Kampuni ya Bia Tanzania Limited kupitia bia yake ya Kilimanjaro, leo hii imekabidhi basi jipya kwa Timu ya Taifa (Taifa Stars), likiwa na thamani ya zaidi ya Sh milioni 200 kwa udhamini wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.

No comments:

Post a Comment