Thursday, December 10, 2009

TUSIJIDANGANYE MIAKA 48 YA UHURU BADO NI
BURE KABISA!!!!





Kama sijakosea ni miaka 48 tokea tupate "Uhuru" na ndoto za wengi bado kutimia. Hivi kweli tuna haja ya kusheherekea kwa chochote? Au ni kaumoja ketu na kutawaliwa na serikali ya CCM kwa miaka hii yote? Au ndio kusema tunaridhika na hali tuliyonayo? Mgao wa umeme, ukosefu wa maji, hali duni ya matibabu, elimu duni, ufisadi uliokithiri, na umasikini ulioshamiri... Watanzania tuamke na kudai zaidi toka kwa hao tuliowaweka madarakani na vile vile tuige kwa wenzetu(kwanini Rwanda wanaweza?). Watanzania mnaokaa mijini msidanganyike na magorofa na maduka makubwa mnayoyaona huko mijini, nendeni vijijini mlikotoka ndio mtaelewa kwamba kumbe bado sana!

1 comment:

  1. Je, na wewe uliyeikimbia na kuitelekeza nchi tukuiteje? Wewe umeifanyia nini nchi hii?

    Baadhi ya viongozi wetu wamejaribu sana na baadhi ya sababu za kushindwa kwa sera zao ziko nje ya uwezo wao. Makosa yapo yametendeka lakini hawakukimbia nchi. Kama kweli una uchungu na nchi yako RUDI kwenu Tanga ukasaidie wazigua wenzio na siyo kukaa Malekani na kubakia kulalamika!

    Happy 48th Birthday Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; na usitishwe na vikaragosi na wasaliti. Safari ni lazima iendelee na tutafika tu!

    ReplyDelete