Thursday, August 28, 2014

Buriani BETTY NDEJEMBI: Tusake #JusticeFor Betty kwa kupambana na unyanyasaji mtandaoni (Cyberbullying) pia


Ninaandika makala hii nikitambua bayana kuwa itamuudhi kila mtu anayeingia mtandaoni kwa minajili ya kuwanyanyasa watu wengine. Lakini siku zote ninaamini katika busara hii: kuuchukia ukweli hakuufanyi kuwa uongo. Ukweli ni ukweli na uongo ni uongo. Ukweli hauwezi kuwa uongo, na kadhalika uongo hauwezi kuwa ukweli. Kamwe asilani.

Wakati tunaomboleza kifo cha ndugu yetu Betty Ndejembi hatuwezi kukwepa ukweli kwamba siku chache kabla ya kifo chake binti huyo alinynyaswa mno kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter. Japo hadi muda huu hatuwezi kuhusisha moja kwa moja uhusiano kati ya unyanyasaji huo na kifo cha binti huyo, ukweli tu kwamba mtu akinyanyaswa masaa kadhaa kabla ya kifo chake, waweza kujenga picha flani.

Naomba ieleweke kuwa simlaumu mtu kwa sababu sina mamlaka ya kufanya hivyo bali dhima ya makala hii ni rambirambi zangu na kuzungumzia tatizo la unyanyasaji mtandaoni, sambamba na suala zima la unafiki kila kinapojiri kifo hususan cha mtu maarufu.

Tuna tatizo kubwa huko mitandaoni. Tumefika hatua ya kuwapa umaarufu watu wenye matusi ya nguoni, wazushi, wambeya, wanafiki, wanaharamu na kila aina ya binaadamu wanaostahili laana lakini twaishia kuwatukuza. Kwa Twitter, matusi imekuwa ni njia ya mkato ya kupata umaarufu. Kuna wenzetu wengi tu wenye 'umaarufu' huko Twitter, na ukidadisi chanzo cha 'umaarufu' huo, utaambiwa 'ah huyu ana matusi si mchezo!'

Kuna watu wazima na akili zao wanatumia muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii aidha kunyanyasa wenzao kama si kusherehesha unyanyasaji huo. Marehemu aliitwa majina kadhaa ya kumdhihaki kabla ya kukutana na mauti. Kuna waliomwita Di Maria na wanajifahamu. Japo sijui chanzo cha 'ugomvi na aliogombana nao' (na ndio maana sikujihusisha nao kwani haukunihusu), kuna wanafiki wengi tu waliokuwa katika nafasi nzuri ya kuzima moto huo hasa kwa vile baadhi yao walikuwa wakizifahamu pande zote mbili za 'ugomvi' husika.


La kukera zaidi ambalo ni wazi litajichomoza wakati wa maombolezo haya ni unafiki: baadhi ya watu walewale waliodiriki kumwandama marehemu wakati wa uhai wake watageuka kuwa wenye uchungu mkubwa baada ya kifo chake. Hii inanikumbusha suala ambalo nimeshawahi kulizungumzia mara kadhaa, katika hali ya utani japo wenye uweli, kwamba 'wakati mwafaka kabisa wa kutafuta vipaji vya uigizaji ni kwenye misiba: watu walewale waliokuwa wakikuchukia kwa nguvu zote watageuka wenye uchungu mkubwa kwa kifo chako.

Ukiangalia baadhi ya tweets za mwisho za marehemu ni wazi kuwa binti huyo alikuwa anahitaji msaada kutoka kwa wanaomjali




Hata pasi uelewa wa taaluma ya saikolojia, tweets za aina hii zinaashiria tatizo, na laiti 'wenye upendo wa dhati' wangeingilia kati muda huo, huenda muda huu Betty asingekuwa marehemu. 


Na hizo tweets mbili ambazo ni miongoni mwa za mwisho kabisa za marehemu ni ushuhuda tosha wa jinsi alivyokuwa akisumbuliwa na wanyanyasaji dhidi yake mtandaoni. Ndio pengine kilichomuua ni maradhi ya kawaida ya kibinadamu lakini kila mwenye ubinadamu hatoshindwa kuhusisha unyanyasaji huu na hali mbaya ya afya aliyokuwa nayo hadi anafariki.

Kuna watakaolaumu kuwa ninatumia kifo cha binti huyo kwa 'maslahi binafsi.' Hapana, sina maslahi yoyote binafsi hasa ikizingatiwa kuwa sikuwa nikifahamiana na marehemu. Hakuna anani-follow na mie sikuwa nam-follow. Labda maslahi pekee niliyonayo ni upinzani wangu mkali dhidi ya unyanyasaji wa mtandaoni. Vyovyote ilivyo, marehemu alikuwa bullied kabla hajafariki na atakayetaka kukataa ukweli huo na akatae lakini utabaki kuwa ukweli usioweza kugeuka uongo. Na kwa hakika, kila aliyeshiriki kumnyanyasa binti huyo atakuwa anasutwa na nafsi yake, hata kama atatafuta hifadhi kwenye 'huu sio wakati wa kulaumiana' au 'we failed you Betty.' 

Mara nyingi nimekuwa nikiwalaumu watu wanaodai 'Instagram imekuwa mbaya' au Twitter imeharibika siku hizi' ambapo mara zote nimewakumbusha wahusika kuwa katika hii mitandao ya kijamii, ni muhimu kuwa makini katika nani wa kum-follow. Maana yangu ni kwamba ukim-follow mtu mwenye matusi, utashuhudia matusi katika anachoandika. Ukim-follow mtu wa busara, utashuhudia busara.

Hata hivyo, katika siku za hivi karibuni kumeibuka kundi kubwa tu la watu wenye busara na elimu zao lakini wepesi wa kuvutiwa na vitu vya 'kipuuzi' - umbeya, matusi, majungu, na upuuzi mwingine, na hawasiti kushea na wanaowa-follow. Ni hivi, mtu akitweet tusi, kisha ukali-retweet, utambue kuwa unalikuza (amplify) tusi hilo. Na kimsingi, kwa kiasi kikubwa, tuna-RT vitu tunavyoviunga mkono. Uki-RT tusi maana yake unaliunga mkono. Na ni wazi mwenye kujiheshimu, na kuheshimu 'watu wa maana' wanaom-follow hawezi ku-RT upuuzi.

Tatizo kubwa sasa ni kwamba waweza kuamua kuwa-follow watu unaodhani wana busara au akili za kutosha lakini ukaishia kusoma vitu vya ajabu ajabu kwenye timeline yako kutokana na haya 'mahaba' ya ku-RT vitu vya kipuuzi. 

Binafsi, nadhani chanzo kikubwa cha mitandao ya kijamii kuwa 'sehemu za kukera, kuogopesha, kunyanyasana, nk' ni ile hali ya baadhi ya wenzetu kutokuwa na vitu muhimu vya kufanya katika maisha yao. Ni wazi kwamba ukiwa busy na maisha yako hutokuwa na muda wa kubughudhi wenzako. 

Kingine kinachopelekea social media kuwa 'dunia uwanja wa fujo' ni ugonjwa mkubwa unawasumbua baadhi ya wenzetu: kusaka sifa wasizostahili. Wanasema,. ashakum si matusi, 'lugha ya mpumbavu ni matusi,' na ndo maana baadhi ya wenzetu wasio na cha maana cha kuongea katika hadhara hukimbili matusi, unyanyasaji, maneno macha

Nitamke bayana kuwa siandiki makala hii nikitegemea kuungwa mkono na wahusika wa unyanyasaji mtandaoni. Na kwa hakika kuna uwezekano mkubwa wa makala hii kuzua 'kampeni ya chuki' dhidi yangu kutokana na makala hii. Tatizo kubwa la wenzetu hawa ni kutotaka kuambiwa kuwa 'Hapana, hili ni kosa. Na kosa ni kosa, haliwezi kuwa sahihi.' Lakini pamoja na uwezekano wa 'kuwashiwa moto' kutokana na makala hii, wito wangu kwa kila mwenye busara na akili ni kuliangalia tukio hili la kusikitisha kama 'wake up call.' Tujifunze, tujisahihishe. Tuache kusherehesha vitu vya kipuuzi mtandaoni.

Ifike mahala, ukishindwa kumkemea mtu mwenye tabia mbaya mtandaoni basi chukua option  rahisi ya kum-unfollow au ikibidi kum-block. Na ifike mahala kuwafahamisha watu wanaoendekeza utoto, majungu, umbeya, unyanyasaji na upuuzi mwingine kuwa kama hawana kitu cha maana cha kufany katika maisha yao basi isiwe sababu ya kuwasumbua wenzao wenye majukumu katika maisha yao.

Tukemee maovu badala ya kutarajia yataondoka yenyewe tu. Tuomboleze kifo cha Betty kwa kusema 'NO' kwa cyberbullies (wanyanyasaji wa mtandaoni). Tufike sehemu tuache kuwasujudia wahuni wanaodhani matusi ni sehemu ya wimbo wa taifa. Tuwakwepe waendekeza majungu, wanyanyasaji, wataka sifa za kipuuzi, na watu wasiofaa katik maisha yetu.


Wakati 'tunatafuta haki kwa marehemu Betty kutokana na unyama aliofanyiwa,' suala ambalo ni la kisheria, kilicho ndani ya uwezo wetu ni kukemea unyanyasaji mtandaoni (cyber bullying). Wakati hadi muda huu hatuwajui waliomfanyia marehemu unyama huo, takriban sote twawajua vema wanyanyasaji wa mtandaoni. Tuanze na hawa, kwani leo wamefanya kwa kwa marehemu Betty kesho itakuwa kwako.

Mwisho kabisa, ni muhimu kwetu sote kutambua kuwa tulitoka kwa udongo na tutarudi kwa udongo. Kifo ni hatma ya kila mmoja wetu.Betty ametutoka lakini nasi twaelekea huko. Visa, chuki, kunyanyasana, na vitu vingine visivyopendeza japo ni kama sehemu ya maisha yetu havipaswi kupewa nafasi katika maisha yetu haya ambayo hakuna mmoja wetu mwenye japo 'lue' ya lini yatafikia kikomo. TUPENDANE na TUHESHIMIANE.

Kwako marehemu Betty, hakuna tunaloweza kusema au kufanya sasa kurejesha uhai wako. Na hakuna neno sahihi la kuonyesha jinsi gani kifo chako kimewagusa wengi. Kubwa tunaloweza kufanya ni kukuombea kwa Mwenyezi Mungu akupatie pumziko la milele na mwanga wa milele akuangazie upumzike kwa amani. Amina.



SKYLIGHT BAND WAZIDI KULITIKISA JIJI LA DAR NA VIUNGA VYAKE KWA BURUDANI KALIII ILIYOKWENDA SHULE


Diva wa Skylight Band Mary Lukos Akiimba kwa uzuri kabisa Ndani ya kiota cha burudani Thai Village.Bendi yako machachari na inayopendwa zaidi ndani ya Jiji la Dar es salaam na viunga vyake vyote Skylight Band inakukaribisha wewe mdau,mpenzi na shabiki wa kweli Leo hii kuanzia mida ya Tatu kamili ndani ya ukumbi wa Thai Village masaki,ambapo burudani ya nguvu itaporomoshwa na wanamuziki mahiri wa bendi hiyo kama Aneth Kushaba,Mary Lukos,Digna Mpera,Sam Machozi,Donode,Joniko Flower na Sony Masamba.Njoo upate muziki mzuriiiii na ladha zote za kiafrika na ulaya pamoja na suprizeee kibaooooo.
Digna Mpera akiimba na kucheza kwa umahiri kabisa ili kuwapa burudani wapenzi na mashabiki wake
Anaitwa Aneth Kushaba A.K.A AK47 au Le Meneja Her Self akiimba kwa mikogooo safi ndani ya Thai Village ili kuwapa burudani ya nguvu Mashabiki wake
Le Meneja Her Self Akiimba kwa Hisia Kaliiiiii Kabisaaaaa
Aneth Kushaba(katikati)akiongoza madiva wenzake wa Skylight Band Digna Mpera(kulia) na Mary Lukos(kushoto) kushambulia jukwaaa sawa sawa na kwa vocal kali
Hashimu Donode A.K.A Dogo Dogo akilishambulia jukwaaa kwa nguvu ili kuwapa burudsni mashabiki wake
Bana ba Kongo Joniko Flower(kushoto) na Sony Masamba(kulia) wakiimba kwa uzuriiiii kabisa zile ladha za kilingala na bolingo na kutoa burudani kaliiii kwa mashabiki wa Skylight Bnd
Hapo sasaaaa Bana ba Kongooo wakianza kuyarudi mauno taratibuuuuuuu
Joniko Flower(kushoto)akiongoza Majembe ya Skylight Band Sony Masamba(katikati) na Sam Mapenzi(kulia)kucheza masebene yaliyokuwa yakiporomoshwa ndani ya Thai Village 
Sony Masamba(kushoto) na Sam Mapenzi(kulia)wakiyarudi kwa rahaaa zaooo
Hapo sasaaa Mpaka chini taratibuuu Joniko Flower(kushoto)akiongoza Majembe ya Skylight Band Sony Masamba(katikati) na Sam Mapenzi(kulia)kucheza masebene yaliyokuwa yakiporomoshwa ndani ya Thai Village 
Hapana chezea kabisa vijana hawaaaaa,si unaona mwenyewe mastepu hayooo njooo leo na wewe ufurahiiii
Hapo sasa Aneth Kushaba Le Meneja Her Self(kulia) Akiwapa tafu ya mauno lainiiiiii na nyoroti Sony Masamba(katikati) na Joniko Flower(kushoto)
Daudi Tumba Akiziadhibu vilivyo tumba zake ili kuleta ladha nzuriiiiiii ya muziki
Tophy bass Akilikung'uta vilivyo Gitaa Lake kuleta ladha tamuuuuuuu kwenye muziki
Mozee Vinanda akifurahia kuzipapasa tufe za kinanda chake na kuleta ladha tamuuuu kwenye muziki unaopigwa
Viunooooo Viunoooooooo hapo ni mashabiki wakicheza kwa raha zaooooo muziki mzuri uliokuwa ukipigwa na vijana wa Skylight Band
Hapo ni viunoooo hatari kwa mashabikii kwa mduara mzitooo uliokuwa ukipigwa
Mwanamanyoya akipata Ukodak na Mdau wa Skylight Band
Wadau wa Skylight Band Wakipata Ukodak kwa Furahaaa teleeeeee
Furaha ya muziki mzuri,ndio maana wadau hawa wa Skylight Band wana Rahaaaaaa
Weweeee na Yuleeeee usikoseeee leo ndani ya Thai village upate burudani nzuriiiiiiii!!!

Viongozi, wanaharakati wataka Katiba Mpya Imtambue mtoto na haki zake

Mwenyekiti wa Mtandao wa Mashirika yanayofanya kazi na Watoto Tanzania ambaye pia ni Mratibu Miradi, Kituo cha Watoto wa Mtaani cha Dogodogo Kigogo (Dogodogo Centre Street Children Trust), Sabas Masawe.[/caption] MCHAKATO wa kujadili na kuandika Katiba Mpya unaendelea bungeni mjini Dodoma, licha ya kuwepo kwa mvutano na mgawanyiko wa makundi ya wabunge wa bunge maalumu wanaojadili Rasimu ya Pili iliyowasilishwa kwao. Wakati hayo yakiendelea viongozi, wanaharakati na wadau wa watoto wanapendekeza masuala ya haki za msingi za watoto yatambulike vizuri katika katiba ijayo. Mwenyekiti wa Mtandao wa Mashirika yanayofanya kazi na Watoto Tanzania ambaye pia ni Mratibu Miradi, Kituo cha Watoto wa Mtaani cha Dogodogo Kigogo (Dogodogo Centre Street Children Trust), Sabas Masawe anashauri ibara ya 43 ambayo inataja haki za msingi za watoto iendelee kuwepo mpaka Katiba inakamilika na iboreshwe zaidi katika mchakato unaoendelea Bungeni. Nasema haya maana tayari kuna baadhi ya watu wameanza kuhoji kwamba kwanini hata watoto wanaingia kwenye katiba ilhali wao ni sehemu ya watu kama wazazi wao. Anasema pamoja na kuingizwa kipengele cha mtoto kwenye rasimu ya pili ya katiba bado kuna mambo ambayo wao kama wadau wangependa yaingizwe tena hivi sasa katika mchakato wa majadiliano unaoendelea. Anasema baadhi ya mambo hayo ni kama umri wa mtoto mwenyewe kutaja wazi kwamba ni kuanzia umri gani. "...Unaweza ukaangalia hili ni suala la msingi sana kutaja umri wa mtoto mwenyewe anayezungumziwa...kwa sisi wadau wa watoto tunashangaa sana kwa maana nyingine tunaona suala hilo ni kama linaongeza utata, kumuweka mtoto kwenye katiba ilhali umeshindwa kumtambua (kiumri) mtoto ni yupi ni sawa na vichekesho...tunashauri mtoto huyu umri utajwe wazi kuondoa utata...," anasema. Mfano ukisema wazee wana haki ya kutibiwa bure lazima useme huyu mzee anaanzia umri gani na kuishia wapi. Huwezi kusema wazee watibiwe bure alafu unashindwa kuainisha vitu vya muhimu kama umri wao, bila hivyo utaleta mkanganyiko wa tafsiri...ndiyo maana hata sasa mtoto anayetajwa tunataka tujue anaanzia umri gani na kuishia umri gani. Sasa hili pekee linatushangaza watu wasomi wanajadili bila kuliona hili.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Fatma Mwasa akizungumza na mwandishi wa makala haya.
Huyu mtoto akiingia kwenye mgongano katika sheria anashughulikiwa namna gani kwasababu hili linaweza kuwa na mgongano kama pia litashindwa kutajwa kwenye katiba chombo ambacho ni sheria mama ya nchi. Masawe anasema mambo mengine ambayo yanatakiwa kuainishwa ni pamoja na kuelekeza namna ya kuwawajibisha wazazi ambao wamekuwa wakikimbia majukumu yao ya kulea watoto na kuwapeleka katika vituo vya yatima eti kwa madai wamewashinda. "Hapa tunataka ijulikane pia hawa wazazi ambao wamekuwa wakikwepa majukumu yao wanawajibishwa vipi...maana wengine tunawapelekea mtoto wake anatamka wazi kwamba mimi huyu mtoto amenishinda kabisa, sasa kama amekushinda nani wa kukulelea? Sasa watu kama hawa lazima ijulikane namna wanavyowajibishwa kwenye katiba au kama ni jukumu la Serikali katiba ieleze wazi ili iwe rahisi kumbana mtu kisheria," anasema Masawe.Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Watoto na Jinsia wa Tanzania, Anna Maembe, anasema Serikali inawapenda watoto na ndiyo maana katika mchakato mzima wa kukusanya maoni ilizingatia kupata maoni ya kutosha kutoka kwa watoto wenyewe pamoja na wadau wengine wanaotetea haki za watoto. Bi. Maembe anasema Ibara ya 43 katika Rasimu ya Pili imeweka wazi haki za watoto pamoja na kufafanua zaidi. "...Ibara ya 43(1) (a) na kuendelea hadi (g) inaongelea kabisa na kufafanua kwa kina haki ya mtoto...hii ni pamoja na kulindwa, kuelimishwa, kupatiwa huduma za afya na huduma zingine zozote muhimu ambazo zitamfanya mtoto akuwe na kufikia utimilifu ambapo naye awe mzalishaji na mwananchi mwema...," anasema Bi. Maembe akizungumza na mwandishi wa makala haya. Anasema katika mchakato wa kukusanya maoni wadau wamepewa nafasi ya kutosha katika kutoa maoni kwa ushirikiano na wabunge, wadau wengine wa watoto, pamoja na mabaraza ya watoto ambayo yapo kila wilaya kutoa sauti za watoto. Anasema anaamini ibara iliyopo sasa inayozungumzia haki za watoto itaboreshwa zaidi mara baada ya mchakato kufikia mwisho hivyo kutoka na mwongozo mzuri zaidi wa kutetea haki za kundi hilo la watoto. "...Binafsi mi bado naamini kuwa mchakato wa katiba, mi naomba niseme hivi mchakato wa katiba ni nafasi nzuri sana ya kuweza kutetea haki za watoto wa Tanzania, kwa kuwa mtoto wa leo ndiyo mbunge wa kesho, kwa hiyo tusipoweka haki zake vizuri hata wabunge wetu wajao hawatakaa wakatimiza wajibu wao vizuri...kwa kuwa sisi wote tulianzia utotoni hadi kufikia hapa, kwa hiyo mchakato wa katiba ufanye mambo yote lakini haki za mtoto zionekane vizuri ili sheria zote za nchi ziweze kupata mwongozo kutoka kwenye katiba yetu inayokuja ambayo ni sheria mama kuweza kutoa haki kwa mtoto.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Watoto na Jinsia wa Tanzania, Anna Maembe akizungumza na mwandishi wa makala haya.[/caption] Hata hivyo anasema mbali na haki za mtoto kuzingatiwa katika Katiba inayokuja bado watoto wanapaswa kuzingatia kuwa haki inakwenda sawa na wajibu, hivyo nao wanapaswa kutimiza wajibu yaani wasome kwa bidii, wakubali kuelekezwa na sio wafanye mambo yao kinyume kwa kuwa wanajua haki zao zimezingatiwa. Mkuu wa Mkoa wa Tabora Fatma Mwasa anaipongeza Serikali kwa kitendo cha kutoa msukumo wa kipekee kwa kuwaingiza watoto katika Katiba Mpya. Anaongeza kuwa Serikali ina kila sababu ya kufanya hivyo maana imeridhia mikataba ya kimataifa kulinda haki za msingi za watoto, ambapo katika mikataba hiyo imeainisha mambo ya msingi ya kuzingatia. Haki ya kuishi, haki ya kupata elimu, haki ya afya haki ya kuudumiwa na kulindwa. Anasema kikubwa ambacho tukiweza kukifanya kikapitishwa katika katiba mpya ambacho kitasaidia kuongeza hatua ambayo Serikali imefikia ni kiongeza umri wa mtoto wa kike kuolewa. Akifafanua zaidi Mwasa anasema suala hilo limekuwa na ajenda kwa muda mrefu hasa tunapopigania masuala ya kijinsia, usawa na haki za watoto. Anasema eneo hili la umri wa kuolewa limekuwa likizua mkanganyiko kwa wengi kwa kile upande mmoja sheria kuruhusu mtoto wa chini ya miaka 18 kuolewa, licha ya upande mwingine bado sheria nyingine inamtambua mtu chini ya umri wa miaka 18 ni mtoto. "...Kimsingi eneo hili limekuwa likizua utata kwa baadhi ya makundi katika jamii...hasa baadhi ya viongozi wa dini wao wanasema mtoto wa Tanzania anamaliza elimu ya msingi akiwa na miaka 14 na hapo kama hakufanikiwa kuendelea na sekondari hubaki nyumbani bila kuwa na cha kufanya, wanasema mtoto huyu anaweza kujiingiza katika mchezo mbaya kama atakaa tu akisubiri umri wa kuolewa wao wanaona kama amepata wa kumuoa ni bora akaolewa kuliko kujikuta akijiingiza katika mambo yasiofaa," anasema Mkuu wa Mkoa huyo. Anasema hata hivyo anaishukuru Serikali kuleta shule za kata maana idadi kubwa ya watoto sasa wanapata nafasi za kuendelea na masomo na kujikuta wakiepukana na hatari za ndoa za utotoni, lakini pamoja na hayo anasema bado kuna haja ya kujenga mfumo mzuri wa kuhakikisha suala la ndoa za utotoni linatoweka kabisa. Pamoja na hayo anabainisha kuwa kuna haja ya Katiba kutamka wazi kuwa mtoto asiruhusiwe kuolewa chini ya umri wa miaka 18. Akizungumzia haki kwa makundi maalum ya watoto wakiwemo walemavu, anawashauri wazazi wenye imani potofu kubadilika na kumchukulia mtoto mlemavu ana haki zote kama ilivyo kwa watoto wengine. Anasema baadhi ya wazazi wamekuwa wakiwaficha watoto wenye ulemavu ili wasiweze kupata haki zao ya msingi. "...Kwenye hili changamoto kubwa ilikuwa wazazi wenyewe kufikiri kuwa kuzaa mtoto mwenye ulemavu ni jambo ambalo linaleta fedheha, hii imekuwa ikisumbua sana maana wakati mwingine tunabaini watoto wenye ulemavu wakiwa wamewekwa ndani wakati mwingine kwa miaka kadhaa...sasa hili tunaamini sio haki maana mtu yeyote anaweza kuwa mlemavu wakati wowote hata mimi sasa kumbagua juu ya haki kwa kuwa yuko vile sio sawa hata kidogo," anasema Mwasa. Bi. Valerie Msoka ni Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanahabari Wanawake (TAMWA), anasema ili mabadiliko katika jamii yatokee vyombo vya habari vinahitajika sana na kwa namna yingine vinatoa mchango mkubwa. Anatolea mfano kuwa kwa sasa matukio ya ndoa za utotoni bado yanashamiri kwa baadhi ya mikoa kwa kiasi kikubwa. Anasema pamoja na vitendo hivyo kuendelea vyombo vya habari ndiyo nyenzo pekee ambayo inaweza kubadili mtazamo katika jamii na matendo hayo kukoma kabisa. Anasema mijadala inayoendelea kutoka kwa jamii na vyombo vya habari kuendelea kuripo inasaidia wajumbe wa Bunge la Katiba kupata taarifa za kina zaidi juu ya masuala mbalimbali wanayoyajadili hivi sasa hivyo kuendelea kuboresha zaidi. "...Mfano masuala ya ndoa za utotoni yanayozungumzwa hivi sasa, ukeketaji na masuala mengine ya unyanyasaji wanayofanyiwa watoto na vyombo vya habari kuandika yanawasaidia wabunge kuwa naufahamu zaidi wanapochangia katika kamati mbalimbali za Bunge la Katiba...kwa maana hiyo mchango wa vyombo vya habari unaitajika sana," anasema Bi. Msoka. Bi. Valerie Msoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanahabari Wanawake (TAMWA). Anasema ili kuondoa utata juu ya umri wa mtoto; Katiba ijayo ingemsaidia mtoto kutamka wazi kuwa mtoto wa kike au wa kiume haruhusiwi kuoa au kuolewa akiwa chini ya miaka 18. Anasema hii ikitamkwa wazi watu wataelewa na hata utoaji elimu kwa jamii juu ya umri wa mtoto na haki zake hauta kuwa wa mkanganyiko kama ilivyo sasa. Anasema kwa sasa zipo baadhi ya mila zinashindwa kumlinda mtoto hasa wa kike hivyo kujikuta wanaozeshwa na kukosa haki zao za msingi ya kupata elimu, ilhali sheria zinashindwa kuwasaidia kwa kile nayo kuwa wa utata juu ya umri wa kuolewa kwa mtoto. Anasema katiba mpya ikitamka wazi masuala hayo itakuwa rahisi kuwashughulikia wanaotumia udhaifu wa sheria na kumnyanyasa mtoto. Hata hivyo anafafanua kuwa pamoja na kuweka sheria ya kumlinda mtoto katika hali zote za unyanyasaji bado jamii inatakiwa kupewa elimu ya kutosha juu ya kuziacha mila na desturi zilizopitwa na wakati ambazo zimekuwa zikimnyanyasa mtoto hasa wa kike. Mwanaharakati huyu ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba anashauri elimu ya kuanzia msingi hadi kidato cha nne itolewe bure na kwa watoto wote. Anasema mtoto atatakiwa kusoma hadi kidato cha nne bure kama ilivyo darasa la saba sasa kisha kuchujwa kidato cha nne. "...Nasema hivyo nikiwa na sababu kwamba ukiangalia mtoto anayemaliza elimu ya msingi madarasa ambayo ni lazima kila mmoja apitie, wanamaliza wakiwa wadogo sana, sasa kwa hali hii mi ninashauri kuanzia msingi hadi kidato cha nne yangekuwa ni madarasa la lazima na bure ili watoto hawa wapate elimu hadi kidato cha nne angalau hapa watakuwa wameongeza kitu kichwani na miaka kusogea...," alisema. Anasema mtoto anayemaliza katika kidato cha nne angalau atakuwa amepata elimu kiasi, anajitambua na umri umeongezeka kidogo hivyo kama wengine wataishia katika darasa hilo wanaweza kujitegemea na hata walioolewa watajitambua hivyo kujenga familia ambazo zinajielewa kwa kiasi fulani tofauti na ilivyo kwa sasa. Kwa upande wake Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Watoto na Jinsia wa Tanzania, Sophia Simba anasema takwimu zinaonesha kuwa Tanzania ni kati ya nchi 20 Ulimwenguni ambazo zimekithiri kwa kuwa na ndoa za utotoni. Aidha anabainisha kuwa takwimu pia zinaeleza katika kila watoto tano, wawili kati yao wameolewa chini ya miaka 18. "...Hili ni tatizo kubwa sana, fikiria kwa kila watoto watano wasichana wawili kati yao wameolewa chini ya miaka 18, sasa ukiangalia utaona karibuni kila wakati kuna mtoto anaolewa Tanzania akiwa chini ya miaka 18. Hili Serikali haiwezi kukaa kimya ndiyo maana kuna programu mbalimbali zinafanywa kukabiliana na hali hii...leo tumezinduwa kampeni za kukabiliana na hali hiyo Mara tutafanya hivi maeneo mengine pia kupinga suala hili," anasema Bi. Simba. Pili Muherisens (13) ni mwanafunzi wa darasa la tano katika moja ya shule za msingi Wilayani Tarime. Binti huyu alilazimika kutoroka kwao na kukimbilia eneo lingine akikwepa kukeketwa na wanaukoo kijijini kwao. Mtoto huyu wala wazazi wake wote hakupenda kukeketwa baada ya kuhofia madhara ya tendo hilo lakini ukoo ulishinikiza na ukatishia kama wazazi watazuia mtoto wao kufanyiwa hivyo wangeliwatenga na mama yake kupigwa. Hapo ndipo binti alipoamua kukimbia kijiji na kwenda kwenye vituo salama. Binti huyu anaomba Serikali iwasaidie watoto kama hawa ambao hulazimishwa kukeketwa na hata kuozeshwa mapema ikiwa ni vitendo vya unyanyasaji dhidi yao. Cha kujiuliza ni watoto wangapi Tanzania ambao wanakumbana na unyanyasaji wa nguvu kama huu. *Imeandaliwa na www.thehabari.com

Saturday, August 23, 2014

Nicki Minaj's dancer 'gets bitten by 6ft long snake' while rehearsing for MTV Video Music Awards

Rehearsal gone wrong: Nicki Minaj's dancer apparently got bitten by a snake during a run-through for Sunday's MTV Video Music Awards on Friday. She is pictured here in May
The website claims the dancer was rushed to hospital after being bitten and is currently receiving medical treatment.
It is believed the snake was an anaconda. The non-venomous reptiles can still cause dangerous infections by spreading bacteria. 
It is unknown if the snake will still be used in the performance, but TMZ reports it was taken away from the run-through in a container after biting Nicki’s dancer.
New song: The singer was rehearsing her performance of Anaconda when the alleged incident occurred
The 31-year-old would not be the first star to appear on stage with a snake at the VMAs.
Britney Spears’ 2001 performance of I’m A Slave 4 U is still famous after she kicked off the song with a yellow python wrapped around her neck.
The VMAs is no stranger to risqué antics on stage, from Britney and Madonna’s liplock in 2003 to Miley Cyrus’ infamous twerking session with Robin Thicke in 2013.
Scary: It is believed the snake was an anaconda. They are not venomous but can cause infections by spreading bacteria
Nicki debuted the very raunchy video for Anaconda earlier this week, and no doubt has been planning a performance that's just as shocking.
Anaconda is Nicki's second single from her upcoming album The Pinkprint, which still does not have a release date.
The record's first track, Pills N Potions, was released in May.
Famous performance: Britney Spears had a python wrapped around her neck while singing I'm A Slave 4 U at the 2001 VMAs.

Grand jury in Ferguson case includes three black jurors and is 75% white The grand jury consists of six white men, three white women, two black women and one black man The ages and hometowns of the jurors weren't released

Prosecutors convened a grand jury to begin hearing evidence in the case, despite concerns among some in the community - including Brown's parents - that the office would not be impartial because of District Attorney Bob McCulloch's ties to law enforcement
McCulloch's father, mother and other relatives worked for St. Louis police, and his father was killed while responding to a call involving a black suspect 
Victim: Michael Brown, pictured, was shot and killed in a August 9 incident by Ferguson police officer Darren Wilson

The fear among some local residents and officials trying to maintain peace in Ferguson is that failure to charge the officer could stoke new anger among a community profoundly mistrustful of the legal system. Many say they just hope the grand jury's decision, whatever it is, has irrefutable facts to back it up.

U.S. Sen. Claire McCaskill told The Associated Press she's pushing for federal and local investigations to be completed around the same time so that all evidence in the case can be made public - a step many consider important should prosecutors decide not to charge the officer. Her office said Friday that the Department of Justice hasn't given a timeline for the federal investigation, which centers on whether a civil rights violation occurred when officer Darren Wilson fatally shot the unarmed Brown Aug. 9.

McCaskill, a former prosecutor in Missouri, said she's hopeful the physical evidence in the case - including blood spatter patterns, clothing and shell casings - will provide "incontrovertible facts" about what happened during the shooting. She said whatever local prosecutors decide, it will be important to explain the decision by providing that physical evidence, and that won't be possible if the federal investigation is ongoing.
Ferguson has been rocked by the shooting. Protesters are seen on August 20 in Clayton, MIssouri
Doubts: Others have questioned District Attorney Bob McCulloch's impartiality in the case 

McCaskill said she urged Attorney General Eric Holder during a meeting earlier this week to speed up what is typically a lengthier federal process.

'What we want to avoid is a decision being made without all the information being available to the public also,' McCaskill said, adding that not being able to do so could 'create more stress and certainly much more fear that we would be back to worrying about people being able to protest safely.'

'Obviously all of us are concerned not just about that this process be fair, but what does this next six months look like?' she said.
Many residents who live in the Ferguson, eager to end the disruptions to their lives caused by protests and police presence, say they fear the community's anger will explode anew if Wilson isn't charged.

'This officer has to be indicted. I'd hate to see what happens if he isn't. The rioting, the looting, man ...,' said resident Larry Loveless, 29, as he stopped at the memorial for Brown where he was killed.

St. Louis County prosecutors this week convened a grand jury to begin hearing evidence in the case, despite concerns among some in the community - including Brown's parents - that the office would not be impartial because of District Attorney Bob McCulloch's ties to law enforcement. McCulloch's father, mother and other relatives worked for St. Louis police, and his father was killed while responding to a call involving a black suspect. He has said he will not remove himself from the case.
The jury hearing evidence in the Michael Brown case consists of six white men, three white women, two black women and one black man

Considering the racial tensions of the case, even the makeup of the grand jury was being closely scrutinized. Two black women and one black man are on the 12-member panel, along with six white men and three white women, said Paul Fox, director of judicial administration for St. Louis County Circuit Court.

Without specifically mentioning the grand jury's racial makeup, the Brown family's attorney, Benjamin Crump, said the panel 'works perfectly' as long as the prosecutor presents the necessary evidence and doesn't withhold information.

Crump said the family doesn't believe the grand jury was necessary, arguing that the prosecutor had sufficient grounds to charge the officer on his own.

The Department of Justice opened a parallel investigation, sending dozens of FBI agents to Ferguson to question witnesses.

Finishing both investigations simultaneously would be unusual because federal investigators typically work independently of their state counterparts and at their own pace, said Paul Cassell, a former federal judge who is a University of Utah law professor.

'That is one of the advantages of a federal investigation. They tend to have a little more distance from the police officers who are being investigated. That provides some assurance of objectivity,' he said.

He said prosecutors must avoid considering the potential reaction - even a violent one - on whether to file charges in any case. He said they must make 'a dispassionate judgment uninfluenced by public opinion.'

The most likely state charges that will be considered in such a case include second-degree murder, voluntary manslaughter and involuntary manslaughter, he said.

Friday, August 22, 2014

Is this Britain's noisiest street? Hundreds of aircraft soar just 40ft above rooftops of Myrtle Avenue at the end of Heathrow's runway


The neat street of semi-detached houses in Hounslow is just a stone's throw from Europe's busiest airport 

It's a popular spot for plane spotters who come from all over the world to watch planes land on the two runways
Road is one of the closest residential streets to the airport's southern runway, with planes flying low over houses
Around 1,280 flights a day come in and out of Heathrow, mostly between 6am and 11pm
An A380 Airbus Super Jumbo comes into land over rooftops at Heathrow Airport South runway
Planes coming in to land over Myrtle Avenue, Hounslow, one of the noisiest streets in Britain
Behemoth: An Emirates planes coming in to land over Myrtle Avenue, Hounslow , believed to be one of the Noisiest Streets in Britain
Neighbours: The road is one of the closest streets to the airport's busy southern runway at just 100 yards from the airport perimeter, with planes regularly flying low over the houses as they jet off and come in to land
Currently there are around 1,280 arrivals flights coming in and out of Heathrow every day, mostly between 6am and 11pm, with the airport alternating the runway used by landing aircraft in a bid to provide noise relief for those living nearby. Airlines are also fined if their planes breach noise restrictions set at 94 decibels during the day, and 87 at night.

Nick Cannon confirms separation from Mariah Carey... but shrugs it off as he accepts the ALS ice bucket challenge

'There is trouble in paradise': Nick Cannon confirmed he and his wife Mariah Carey have been living separately after six years of marriage 
Mariah Carey & Nick Cannon over the years
Speaking with The Insider Cannon explained,:'There is trouble in paradise…we have been living in separate houses for a few months.' 
After shooting down rumours that cheating caused the break, the star said his three-year-old twins are his 'main focus'. 
Then on the same day his interview was released, Cannon posted a video to his Twitter where he accepted the ALS ice bucket challenge in nothing but a towel.

Coming through: The star accepted the ice bucket challenge wearing nothing but a towel
Nick Cannon completes the ALS Ice Bucket Challenge in a towel
He had promised to enact the charitable dare naked, but compromised with the wrap around his waist.

The occasional actor challenged the remaining AGT judges Howard Stern and Howie Mandel as well as Shaquille O'Neal.
Meanwhile, TMZ.com reported his wife was furious when Nick revealed a list of five celebrities he had slept with during a very candid interview with Power 106 radio.

Mariah was left feeling 'humiliated' following the interview, which also featured him revealing when he first had sex with his wife.
Famous ex: Nick briefly dated Kim Kardashian back in 2006 - between her 1st and 2nd marriage
The couple are reported to have separated back in May and have been secretly working out a property settlement and custody agreement over their twins with their lawyers, according to the gossip website.

Sources close to the couple say their marriage started to unravel in March following Nick's interview, when he reflected on his short romance with Kim back in 2006.

He claimed he had too many ex-lovers to list them all, saying: 'Are you kidding me this is L.A.? That's the whole purpose of it, you have sex with actresses, singers, models.'
Untroubled: The star looked to be in high spirits last week while filming AGT in New York
When told he could just name five, the star had his list ready: 'That's easy. OK, Mariah Carey, Christina Milian, Nicole Scherzinger, Selita Ebanks, oh, Kim Kardashian.'

He then elaborated about Kim, now married to rapper Kanye West, saying: 'You just forgot (about her) because there have been a lot of people since me.'

In an interview with another station a week later, he tried to backtrack over his comments and praised his wife's sex skills.

He said: 'She doesn’t even know who Kim Kardashian is. She doesn’t pay attention to that.

'She doesn’t care when I talk about our sex life because our sex life is amazing.'

Looks pretty red hot to us! Kim Kardashian shows off her fabulous curves in a bikini... after complaining she needs to lose 20lbs


Red hot: Kim Kardashian shows off her fabulous curves in a red bikini on holiday in Punta Mita, Mexico
Watersports: The mother-of-one enjoyed a spot of paddle boarding during her vacation
Accompanied by her assistant Stephanie, the reality star enjoyed a spot of paddle boarding.

After trying to paddle on the same board, the pair ended up losing their balance and falling into the sea.

So after their stumble, they wisely decided to paddle along while sitting instead.
Looking good: Despite Kim's complaints she needed to lose more weight, the reality star looked pretty fabulous
This is the life: Kim escaped to Mexico for a few days over the weekend
Nothing to worry about: Despite her insecurities over her body, many of her fans don't seem to agree
The curvy pin-up looked toned and tanned as she played in the sea, despite her recent insecurities over her figure.

Earlier this month, she admitted on Twitter her body wasn't back to her pre-baby weight.

She tweeted: 'Can't seem to shake this last 15-20 lbs of baby weight. No more excuses. My baby is 1 years old! UGH.
Where's Kanye? It looked like the rapper remained on dry land for the watersport session
Double OO heaven: Kim does her best Bond girl impression as she emerges from the sea
This is fun: Kim and Stephanie try to move across the waves on the boards...
Oops! The women lose their balance and fall into the sea
Balancing act: The reality star and her assistant try to keep their balance
'I'm not gonna call it baby weight bc that's an excuse. I just gained weight and that's it. Why is it so much harder to lose after baby though!!

'Do any of u moms see their bodies just not the same? A different shape?

'Ughhhh my hips & butt are huge now! They were big to begin with! Just need to get down to my weight a few years ago. Not gonna complain anymore. Starting diet today! No carbs. crazy workouts. Whos with me?'
'No carbs!' Kim has vowed to stay away from carbohydrates, blaming her weight gain on her love of them
Maybe we should sit down instead? Kim and Stephanie decide to sit down after standing didn't work out so well
Girls time: Despite being in Mexico with her husband, it appeared maybe Kanye wasn't such a fan of the water
Hang time: All that paddle boarding was hard work so the women had a little lounge on the boards
Insecure: The reality star claims she needs to lose another 15-20 pounds
Kim, husband Kanye West and a few friends stayed at close friend Joe Francis's private beachfront villa Casa Aramara, which usually costs $15,000-a-night in low season.

During her trip, Kim posted several photos to Instagram and gushed about her love for the resort.

She wrote: 'Bye Mexico! Every time we come it's a new set of memories & I'm grateful. Thank you Casa Aramara.'
Cheeky: The star had a brief bikini malfunction
Hang 10: Kim is a frequent visitor to Mexico, often popping across the border for a weekend break
Easy does it: Kim looks like she's concentrating hard as she tries to stay afloat
Need a helping hand? Kim drags the board down to the waterfront