Friday, November 29, 2013

That's one gorgeous gene pool! Sam and Billie Faiers look just like their youthful mum in co-ordinating bikini pictures


Bikini babes: Billie, (left) Sam (centre) and mum Suzanne, (right) look like sisters as they take a dip in their swimwear
Looking good: Billie (left), Sam (centre) and Suzanne (right) looked toned as they showcased their enviable bodies on holiday
Many happy returns: The girls were celebrating Ferne McCann's mum, Gill's birthday in the Dubai sunshine
Who's the mum? Sam (left) and Suzanne (right) have a tactile moment in the pool together
Babewatch: No doubt Sam (far left) was glad to get some sunshine after turning down an offer to join her former flame Joey Essex in the jungle
Model behaviour: The girls shared a giggle over something they had seen

THANKSGIVING PARTY NEW YORK MAMBO YALIKUWA KAMA HIVI

 Dj Bilal akiwarusha kwenye party hiyo kama kawaida hakukaa mtu hapa kwa ngoma zake mchanganyiko 
Fundi akiwa na mama mwenye nyumba wake pongezi kwao kwa kufanikisha pati hiyo watu walifurahi kwa kula na kucheza. Hii siyo mala ya kwanza kufanya hivyo na ndiyo maana kila anavyotangaza kukutana kwake kila mtu anajua anachoenda kukipata ni kula kunywa mwanzo mwisho.
 Mambo yalikuwa kama hivi mwendo wa kunesa nesa tu mwanzo mwisho
 Ulikuwa usiku wa kupendeza na pongezi kwa brother Fundi kwa kufanikisha pati hii na watu wakajitokeza kwa wengi.
 kila mtu alikuwa busy
 Watanzania wa jiji la wasiyo lala New York ndiyo habari yenyewe
 Palikuwa hapatoshi kila mtu alipata kitu roho inapenda

 Mambo ndiyo kama hivi muziki hauna utu uzima uzuka ukikupanda mambo huwa kama hivi, Kwa taswira zaidi nenda soma zaidi




Thursday, November 28, 2013

DADA AKIMUONYESHA MWANAE SEHEMU NYETI

Mtoto bila kujua hiki nini, akionekana mwenye mshangao mkubwa au mwenye shauku ya kujua zaidi. Mama yake nae bila hata aibu akirusha mguu mmoja juu ilimwanae apate picha kamili, hii si laana jamani..!! NO NO NO NOMA SANA...!!

TANZANIA, CONGO NA BURUNDI WAUNDA MUUNGANO WAO BAADA YA KUTENGENGWA

Wakati Kenya, Rwanda na Uganda zimeunda umoja unaoitwa `Umoja wa Walio Tayari’ , Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) nazo zimeanzisha ushirikiano baina yao.
Katika siku za karibuni kumekuwa na mtikisiko ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) baada ya Tanzania na Burundi kutengwa na wenzao wa Kenya, Rwanda na Uganda katika baadhi ya masuala muhimu ya ushirikiano hasa wa kiuchumi.
Tanzania, Burundi na DRC nazo zimekutana ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta ambaye aliliambia Bunge lililopita kuwa Tanzania inafikiria kushirikiana na nchi hizo.
Mkutano wa ujirani mwema
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mkutano wa Ujirani Mwema uliofanyika mjini Bujumbura, Burundi jana, Sitta alisema Tanzania, Burundi na Kongo zimekubaliana kuendeleza miundombinu ya barabara, reli, anga na usafiri wa maji katika Ziwa Tanganyika.
Alisema mkutano huo ulilenga kuboresha miundombinu ya usafiri katika Ziwa Tanganyika ambalo linaziunganisha Burundi Tanzania, DRC na Zambia.
“Pia tumepanga kuendeleza reli ya kati kutoka eneo la Uvinza, Tanzania hadi Msongati, Burundi na pia kuunganisha Barabara ya Manyoni - Tabora - Kigoma kupitia Bujumbura hadi Kivu ya Kusini, DRC,” alisema Sitta.
Mkutano huo ulihudhuriwa na Sitta pamoja na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Burundi, Leontine Nzeyimana na Waziri wa Uchukuzi wa DRC, Jack Lukeba.
“Pia tulitembelea Bandari ya Kalindo iliyoko katika Ziwa Tanganyika upande wa Burundi kwani tunataka kuboresha bandari za ziwa hilo,” alisema Sitta.
Waziri huyo alisema Tanzania na Burundi zitaunganishwa na Barabara ya Manyoni – Tabora - Kigoma na Barabara ya Manyovu - Mgina, Mabanda - Bujumbura itakayounganishwa mpaka Kivu ya Kusini, DRC.
Kuhusu usafiri wa anga, Sitta alisema nchi hizo zinaangalia uwezekano wa kuanzisha safari za ndege za Dar es Salaam mpaka Bujumbura.

WASTARA"SINA MAHUSIANO YOYOTE NA MR BOND NAJUTAAA"

Juzi na jana kulikuwa na habari katika gazeti na mitandao mingi kuwa Wastara na Bond Bin Suleiman ni wapenzi na wamekuwa wakifanya siri sana huo uhusiano wao. Habari ambazo zilinukuu chanzo kimoja zilieanda mbali zaidi zikisema huenda Bond ana tabia ya kufanya mapenzi na mwanamke kotekote kwani aliyekuwa mpenzi wake wa zamani Lulu Semagongo(Anti Lulu) alidaiwa kuwahi kukaririwa akisema kuwa anapenda sana kufanya mapenzi kinyume na maumbile na hawezi kuacha tabia hiyo. 

Baada ya habari hizo kusambaa ilibidi blog yetu kuwatafuta mastaa hao wawili na wa kwanza kupatikana alikuwa ni Wastara na alikana kuwa katika penzi na Bond ila alisema wanafanya kazi pamoja kwani kwasasa wanashuti filamu mpya ya Bond inaitwa Uaminifu Dhaifu. Aliongeza kwa kusema kuwa Bond ni kama kaka yake. "sina mahusiano na Bond zaidi ya kikazi tu na zile picha zote ambazo unaziona ni wakati tupo location tukiandaa filamu yake inaitwa Uaminifu Dhaifu, huo ndiyo ukweli, bora mume wangu angekuwepo haya yote yasingetokea

Baada ya hapo ilibidi kumgeukia Bond ambaye yupo location wakimalizia filamu hiyo na alipoelezewa hayo alisema hana uhusiano wa kimapenzi na Wastara na picha zinazodaiwa kuwa ni wapenzi ni za filamu mpya ambayo tuliweka hata hapa katika blog yetu, alisema kuwa huyo Anti Lulu anatafuta kuandikwa tu kwenye magazeti ndiyo maana anatoa habari hizo zisizo za kweli ili kujipatia umaarufu "Sio kweli ni picha za kazi tu ambazo hata wewe nilikutumia magazeti yanazigeuza, Lulu achana nae anatafuta kuandikwa, tulishachana kitambo wala hatuna mawasiliano.

AMA KWELI DUNIA INA MAMBO!......KIJANA MIAKA 32 ANASWA NA BIBI KIZEE MIAKA 80, LOL!... CHEKI MWENYEWE HAPA

Hamad Issa (32) akiwa amejilaza kitandani kwa bibi Adela Mkalau (80).

Tukio hilo la kustaajabisha limetokea mwishoni mwa wiki iliyopita, nyumbani kwa bibi huyo, Yombo –Buza, jijini Dar es Salaam ambapo wajukuu wa bibi huyo ndiyo waliomnasa.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, wajukuu wa bibi huyo walifedheheshwa na kitendo hicho hivyo kuwawekea mtego na kuwanasa kisha kumfikisha Hamad katika Kituo cha Polisi Chang’ombe kwa tuhuma za ubakaji.
Bibi Adela Mkalau (80) akiwa katika pozi.

BIBI: SIJABAKWA
Katika kutafuta uhakika wa madai ya wajukuu hao, polisi wa Chang’ombe waliagiza bibi yao aitwe ili athibitishe madai hayo wakati upelelezi mwingine ukiendelea.
Sosi wetu alisema kuwa bibi aliwaacha hoi polisi baada ya kufika kituoni hapo na kukataa maelezo ya wajukuu zake, huku akisisitiza hakubakwa bali walikubaliana na Hamad.

Baada ya bibi huyo kuondoa utata, polisi walikubali kumuachia Hamad kisha wajukuu wakafunguliwa kesi ya kushambulia na kudhuru mwili iliyoandikishwa kituoni hapo kwa jalada namba CHA/RB/10629/2013.

Hamad Issa akiwa kitandani, pembeni kulia ni bibi Adela Mkalau.

BIBI NA RISASI
Risasi Mchanganyiko lilifunga safari hadi nyumbani kwa bibi huyo na kuzungumza naye kuhusu tukio hilo ambapo alisema: “Sijabakwa na nimekasirishwa sana kwa kitendo cha kumpiga kijana wangu. Wawe na heshima kwa babu yao. Sisi tunapendana, kwa nini wanatuingilia?”
Alisema: “Siku hiyo Hamad wangu alikuja nyumbani kwangu tangu mapema. Nikaandaa chakula cha jioni, tukala pamoja kisha tukalala.

“Tukiwa usingizini, nikasikia mlango unagongwa. Kwenda kufungua, wajukuu zangu wakaingia na kuanza kumpiga Hamad na fimbo na magongo, wakisema eti amenibaka. Hamad atanibakaje? Kwani mimi ni mtoto mdogo?
“Isitoshe wanamfahamu vizuri sana Hamad. Nipo naye mwaka mmoja na nusu sasa, leo inakuwaje wanajifanya hawamjui? Siku hizi mambo yamebadilika. Mdogo anaweza kumpenda mkubwa na mkubwa akampenda mdogo. Hakuna kosa.”
Adela Mkalau akiwa kwa bibi.

MSIKIE DOGO
Mwandishi wetu alikwenda nyumbani kwa Hamad ambapo alimkuta akiwa hoi kitandani kwa majeraha ambapo alisema: “Ni kweli bibi ni mpenzi wangu... na wale wajukuu zake wananifahamu vizuri sana. Wamenipiga sana, eti nimembaka bibi yao. Siyo kweli. Sisi ni wapenzi.”

Alipoulizwa anajisikiaje kuwa kwenye uhusiano na kikongwe huyo, alijibu: “Hata mimi nashangaa sijui imekuwaje nikampenda. Nimejikuta nipo kwenye uhusiano naye na kwa kweli tunapendana sana.”

WAJUKUU WANASEMAJE?
Mmoja wa wajukuu wa bibi huyo, Margaret Cheba, akizungumza na gazeti hili kuhusu tukio hilo alisema bibi yao amewadhalilisha sana na wanaona aibu kupita mitaani kwa kitendo cha kutembea na Hamad.

“Hili jambo limetufedhehesha sana sisi wajukuu zake halafu hata kimila ni tatizo, hairuhusiwi kabisa. Mbaya zaidi, bibi yetu ni mgonjwa. Anasumbuliwa na moyo... sio wa kufanya kitendo kama kile kabisa na sisi ndiyo tunamsaidia lakini inashangaza polisi wametubadilikia kabisa,” alisema Cheba.