Thursday, July 30, 2009











Hali ya usalama kwa watumiaji wa daraja hili(mto Wami) bado ni ya utata sana. Hivi ni lini litaanza kushughulikiwa?



Vipoteza wakati....

Wednesday, July 29, 2009

Monday, July 27, 2009

MAMBO YA BONGO

Nilipokuwa kwenye likizo yangu niliona mambo/vitu ambavyo vimenifanya nijiulize maswali mengi bila kuwa na majibu.
1. Nilishangazwa sana na jinsi sehemu za starehe(mabaa) wanavyofurika watu katika siku zote za juma(Jumatatu mpaka Jumatatu). Je! hii ina maana ya kwamba uwezo wa watu kifedha ni mkubwa sana au pengine tumegeuka kuwa Taifa la walevi? Au pengine starehe ndio shughuli yetu kubwa na muhimu kuliko kitu kingine. Tukumbuke ya kuwa mtindo huu vile vile unaandamana na mambo mengi yanayochangia kwenye kuiangamiza jamii na kurudisha au kuchelewesha maendeleo ya kweli.

2. Nilishangazwa na jinsi makampuni ya simu yalivyotanda na mabango yao ya matangazo karibu kila sehemu, lakini ni mara chache unaweza ukakutana na mabango ya kutukumbusha kuhusu ukimwi kama vile sio tatizo tena Tanzania.

3. Uongozi wa serikali na chama katika Jiji la Tanga umezorota na unachangia sana katika kukwamisha maendeleo ya Jiji hilo(ambalo hata hadhi ya kuitwa Jiji halina). Waarabu wa Tanga si wapenda maendeleo, na ndugu zangu wa Kidigo itatubidi tuchangamke kama tunataka maendeleo.
4. Wanaoiba si kwamba wanaiibia serikali bali ni sisi sote hivyo tusikubali...






Kwa ndugu zangu mlio nje ya nchi yetu tukufu kwa kipindi kirefu ni vizuri tukakumbushana jinsi fedha yetu ya madafu inavyofanana. Kwani kuanzia uhuru mpaka wa leo imeshabadilishwa mara nyingi tu, na si ajabu siku utakayoamua kurudi ukakutana na mjanja atakayetaka kukubambiza na zile zisizotumika tena.



Kuuliza si ujinga... hivi ni nani ana umiliki na jina la mlima wetu wa Kilimanjaro? Je! biashara zinazotumia jina hili, zinahitaji idhini au ndiyo haki yetu sote?

Tuesday, July 21, 2009


Mwanamziki Ras Makunja aka Bw.Kichwa Ngumu na mzimu wake FFU ,juzi jumamosi walifungua ukurasa mpya katika jukwaa la Fest-Africa,kwani waliweza kuwapa burudani ya aina washabiki wa ufini,
wanamziki washambuliaji (FFU) wa safu ya mbele waliweza kuwamdudu washabiki vizuri,Ras Makunja kiwaongoza jukwaani washambuliaji wake wa safu ya mbele mpiga solo Chris-B,ambaye pia anaimba na Bi.Severne aka Sevasha au afande wa kike,huku mdundo mkali wa The Ngoma Africa Band ukiwasindikiza na kuweza kufanikiwa kuwayumbisha washabiki katika onyesho hilo!
Kitu cha kufurahisha mziki huo wa Ngoma Africa uliweza kuwazoa washabiki na kupanda jukwaani kusakata ngoma za moto! mojawapo ya walivutwa jukwaa ni "Mzee Mponda" au tumwite "Dady Mponda" alipanda jukwaani na akawashangaza maelfu ya washabiki kuwa "kuwa wazee wa Kiafrika" wanajua kucheza mziki na kutoa ushindani kwa vijana!
wasikilize ngoma afrika hapa
http://www.myspace.com/thengomaafrica




Ka-vacation katamu...

Jumba la kisasa la mambo ya movies ndani ya Bongo Dar es salaam...

Ukiwa Bongo unapaswa kuwa mwangalifu kuhusu kituo kipi cha mafuta upate huduma, kwani vituo vingi vina mchezo wa kuchanganya mafuta ya taa na dizeli au petroli ili kupata faida zaidi. Vituo ambavyo bado havina sifa hiyo mbaya ni hivi vya BP.


Mnara wa makumbusho ya Azimio la Arusha unasimama kama kitambulisho kikuu cha Jiji la Arusha.

Monday, July 20, 2009

Biashara kando kando ya barabara ya kuelekea Bagamoyo.

Bongo siku hizi kuna kila aina ya usafiri wa haraka haraka chaguo ni lako. Pichani jamaa wa mapikipiki na bajaji wakisubiri abiria.

Sunday, July 19, 2009

Sehemu maarufu jijini Dar - Jolly Club na Las Vegas Casino. Kiza kikitanda sehemu hii huwa balaa tupu!




Tukiwa Dar na Mzee Kombo(baba) na mama mdogo. Wazazi wote walifurahia sana kuwa na wajukuu na wototo nao wamefurahi sana.



Lango kuu la kuingilia Break Point ya mjini. Hapa kuna msosi wa nguvu na ni mahali pa kukutanikia wakati wa chakula cha mchana kwa wadau wengi wa Jiji.
Club Bilicanas inavyoonekana kwa nje.