Wednesday, March 31, 2010

Hii safi sanaaa!! Labda zikiwepo kwenye kila sehemu zinazotumiwa kwa tendo la ngono, pengine itasaidia kupunguza maambukizo ya gonjwa la ukimwi. Nadhani itawaondolea haya wale wanaokuwa wazito kununua toka madukani.
LAILA ALLI
"Like father, like daughter"

Waliowahi kupambana na huyu dada kwenye ulingo watakwambia kwamba sura yake ya kuvutia ni tofauti kabisa na anavyoyatupa masumbwi. Mrembo huyu amewahi kuwahadhibu vibaya sana wapinzani wake ulingoni na kujipatia sifa kama mmoja wa mabondia bora wa kike Duniani.


"THE GREATEST"  NOW AND THEN



Friday, March 26, 2010

Hii sehemu ya kugongewa idhini ya kuingia nchini(Visa) katika Kiwanja cha ndege cha Kimataifa(?) cha Mwalimu Nyerere ina utata kidogo. Kwanza, hakuna kipoza hewa na katika majira kama haya kunakuwa na joto la ajabu. Pili, ni padogo mno kuweza kuhimili abiria wengi na Tatu, bado baadhi ya hawa askari wa Uhamiaji na wa ushuru wana usumbufu usio wa lazima. Labda kwa sisi wenyeji tumeshayazoea hayo, lakini kwa wageni ambao tunataka sana waje nchini mwetu mtazamo wao ni tofauti kabisa. Kama bado tunataka waendelee kuja kwa wingi zaidi, basi tunahitaji mabadiliko. Tukumbuke kuwa wageni hawa wanapoondoka na kuizungumza vizuri nchi yetu kwa jamaa na warafiki zao ndivyo watakavyokuja kwa wingi zaidi.
Inafurahisha sana kuona nyuso za furaha za Taifa letu la kesho. Lakini je, nyuso hizi watakuwa nazo katika miaka Thelathini ijayo? Mategemeo ya wengi ni kwamba watoto hawa hawatakuwa na maisha ya kuangaika kama ya wazazi wao walio wengi. Waliobebeshwa majukumu ya kuliongoza taifa hili inawabidi waache ubinafsi na kuweka ahadi kwamba Tanzania ya kesho isifanane kabisa na ya leo.  Kila kiongozi inabidi awajibike!!!!
Unapotembelea Jiji letu la Arusha, sehemu mojawapo ambayo sio rahisi kutoipitia au kusikia ikizungumziwa ni Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha(AICC). Kuwepo kwake katika jiji hili kumesaidia sana katika kila namna kulijenga jiji hili. Ni nini kitafuatia baada ya mgogoro wa Rwanda kuisha?

Wednesday, March 24, 2010

A 6-year-old boy displays his hands and feet at a hospital in Shenyang, Liaoning province, March 19, 2010. The boy, who has 15 fingers and 16 toes, is scheduled for surgery on Tuesday to remove the extra fingers and toes, local media reported. Experts said a gene mutation contributed to the aberrance.

Blogger Buzz: Blogger integrates with Amazon Associates

Blogger Buzz: Blogger integrates with Amazon Associates
Kwa kweli mji wetu wa Mwanza unaendelea kupendeza sana. Ni lazima tuwape hongera wazee wa "The Rock City" kwa kuuweka mji katika hali ya usafi. Kama yanawezekana Mwanza na Arusha, hivi ni kwa nini Tanga wameshindwa? Hadhi ya kuwa jiji Tanga bado... na huo ndio ukweli!!!!
San Blas Half Marathon (Coamo, Puerto Rico) 1984. The leaders: Zacaria Barie (25) and Gidamis Shahanga (26) from Tanzania, and Mike Musyoki from Kenya. Hardly seen in the back is Marti Vainio from Finland. Barie won the race in 1:04:53, Shahanga  second in 1:05:12 and Musyoki third in 1:05:35. Vainio finished 31th with 1:12:06

Enzi hizo katika riadha Tanzania tulikuwa wakali sana na hata majirani zetu walikuwa wanajua hivyo! Kilichotokea baada ya hapo hamna anayejua.

Tuesday, March 23, 2010

Jamaa akisubiri kwa hamu abiria watinge kwenye kibajaji chake jijini New York.
Urembo

Jlo

Halle B.

Beyonce
Kumbe Urembo ni vipodozi!!!!!!

Saturday, March 20, 2010

Dar 1997 tukila ngano na Elias Mhegera na Eugene Kahigi!!!
Baada ya unyama na ukatili aliowafanyia Waganda, ndipo Amin atambua kwamba kumbe Mungu yupo. Kujitia kuukumbatia Uislamu baada ya maovu yote hayo ni kuipa jina baya dini ya Kiislamu. Sielewi ni kwa nini Waarabu walimuifadhi huyu nduli mpaka mauti yalipomkuta. Wasingempokea kabisa bali wangelimrudisha Uganda apate hukumu yake.
A-Town enzi hizo mambo yote yalikuwa ni Dj Marcop(marehemu) wa kwanza kushoto. Wengine katika picha ni Teddy? mcharaza keyboard wa Tatunane, Fundi na baharia Nuru.
MALAWI CHURCHES: SAME SEX ACTS "SINFUL"

Malawi church leaders say that homosexuality is "sinful" and urge Western nations to withdraw threats to halt
aid to this southern Africa country over a court case that could send two gay men to jail for up to 14 years.




Bishop Joseph Bvumbwe, head of the Malawi Council of Churches, says a three day meeting of the main Protestant groups unanimously agreed Friday to oppose any easing of laws criminalizing same-sex partnerships.



A verdict will be delivered March 29 on Steven Monjeza and Tiwonge Chimbalanga, arrested and jailed since Dec. 26 after holding a public engagement ceremony.


The arrests have outraged human rights groups and Western donors in Malawi, one of Africa's poorest nations. The churches say the West should not be allowed to use its financial power to force Malawi to accept homosexuality.

Friday, March 19, 2010

Moja ya Hoteli za siku nyingi jijini Arusha ni hii ya New Safari Hotel. Zamani kwenye miaka ya themanini ilivuma sana na disco lake "The Cave Disco" ambapo kwa wale wapenda starehe ndipo kulikuwa mahali pa kukutania enzi hizo.

Vijana tukiwa tayari kuingia "The Cave Disco" enzi hizo. Kutoka kushoto, Fundi, Santina na Matare.
Kwa kweli Wabongo tulimpenda George Bush...

Thursday, March 18, 2010


Picha za ndani na nje ya Wanja letu la ndege la kimataifa la Mwalimu Nyerere!
Sehemu ya wanaoingia nchini hairidhishi kama ilivyo wakati wa kutoka. Wakati kama huu wa joto kali ni balaa tupu!!!

Baadhi ya wachezaji wa timu zitakazoshiriki kwenye kombe la mpira kule Afrika ya Kusini wakionyesha jezi za nchi zao watakazozitumia wakati wa michuano hiyo.
Wakati kukiwa kumesalia miezi kama mitatu kabla ya mashindano ya kombe la mpira wa Dunia, mchezaji maashuhuri wa Uingereza, David Beckham hatoweza tena kuichezea nchi yake kutokana na kuumia mguu ambao inabidi upate visu.