Friday, May 21, 2010

Sio lazima uwe na akili nyingi kuelewa kuwa tatizo la fujo na misongamano mijini mwetu(Bongo), inatokana na tulivyoruhusu kiholela vijibasi(Daladala) kutawala mabarabara ya miji yetu kana kwamba ndio vimekuwa mkombozi wa tatizo la usafiri. Nakumbuka wakati tulipokuwa na UDA pale Dar enzi hizo, angalau hali  ilikuwa inafanana fanana na picha za hapo juu. Kulikuwa na kaustaarabu ka aina fulani. Labda pengine, tufikirie tena kuwa na mashirika kama UDA na tuondokane kabisa na hili balaa!

2 comments:

  1. Lakini tukumbuke pia watu dar wameongezeka sana maradufu! UDA pekee halitatatua tatizo lililopo, inabidi watu wakubali kuishi miji mingine pia!

    ReplyDelete
  2. Ninachosema mimi ni kwamba basi kama ni hivyo ni bora tuya-regulate ipasavyo na isiwe kiholela kama ilivyo sasa. Nadhani hivyo vidaladala viko vingi sana na hata hao madereva ni wakutia mashaka. Kama regulations ni za wasiwasi basi matokeo yake ni chaos kama ilivyo sasa.Tatizo la watu kuzidi kuongezeka Dar pia linatokana na mipango duni ya kusambaza huduma muhimu kwenye sehumu nyingine za nchi yetu. Vile vile tunaendelea kuipuuzia miji mingine ambayo pengine ingesaidia kuondoa hili tatizo. Mfano ni mji wa Tanga ambao una-potential ya kila aina, lakini karibu kila kitu kimekufa - siyo bandari wala reli...

    ReplyDelete