Wednesday, April 6, 2011

Mji wa Aschaffenburg,Ujerumani kufungua msimu kwa AFRIKA FEST


Wakazi wa mji wa Aschaffenburg,nchini Ujerumani wanatarajia kufungua msimu wa siku za joto kwa

sherehe za AFRIKA FEST, mjini Aschaffenburg,huko nchini ujerumani aka Ujeuri man.

Shamra shamra hizo za asiye na mwana abebe jiwe ,zinatarijiwa kuanza siku ya tarehe14 April hadi

16 April 2011,ambapo kutakuwa na maonyesho mbali mbali ya sanaa,mziki na utamaduni kwa ujumla.

Na bendera ya Tanzania piga ua inawakilishwa na Dj maarufu "Mfundo pita"ambaye mwaka jana tu

alitajwa na redio mabali mbali nchini ujerumani kuwa ni DJ "Mkali wa midundo" ya World beat.

Mji wa Aschaffenburg,nchini Ujerumani mwaka huu 2011 ndio mji wa mwanzo kufungua dimba

la sherehe za msimu wa joto nchini humo,sherehe hizo zinatarajiwa kuudhuriwa na maelfu ya

wa watu kutoka kila kona ya ujerumani,

Mnakaribishwa wote..

kwa maelezo zaidi wasiliana simu +49(0)1733779720 au ndani ya ujerumani pia

01733779720


No comments:

Post a Comment