Saturday, August 27, 2011

MALI NA MAKAZI YA WANAKIJIJI WAPATAO 200 Kimbiji zimeharibiwa

NANI ? ALEYATOA AMRI YA KUWAVUNJIA MAKAZI NA KUWAHARIBIA MAZAO
WANAKIJIJI KIMBIJI ??


Wanakijiji wa kimbiji bado wamebaki na mshangao ! hakuna afisa wowote wa serikali,kuanzia wilaya,mkoa hadi serikali kuu aliyekwenda kuangalia uharibifu! wala kutoa tamko lolote la kuwalinda wanakijiji !

Uvamizi wa wanajeshi dhidi ya wanakijiji Kimbiji !  Polisi hawajakubali kupokea malalamiko ya wanakijiji ! nani ? wa kumfunga simba kengele?

Uvamizi uliofanyika 16.08.2011 jumanne saa 4.00 hasubui wakazi kijiji cha Kimbiji,nje kidogo ya jiji la Dar, wamekuwa na mashaka ya maisha baada ya makazi na mazao yao kuharibiwa vibaya na wanajeshi (JWTZ) ambao walivamia kijiji hiko na kuvunja vunja makazi ya raia..kinyume cha sheria.

Hata hivyo baadhi ya wanakijiji walipereka taarifa katika vya vituo vya polisi vya Kigamboni na mji mwema,havijakubali kupokea malalamiko ya wanachi walioharibiwa mali zao na kutishiwa usalama wao,hadi sasa inaonekana kuwa wanachi wa Kimbiji hawana wa kuwalinda wao na mali zao,kama inavyoeleza katiba ya nchi kuwa kila raia ana haki ya kupewa ulinzi wa maisha yake na mali zake!

Katika Sakata hili la wanajeshi (JWTZ) kuvamia makazi ya raia na kuharibu mali za raia
bado lina utata wa nani ? kumfunga kengengele simba?

Pamoja na ujangili huo uliofanywa na wanajeshi hao dhidi ya wanakijiji cha kimbiji hakuna uongozi wowote wa ngazi ya wilaya au taifa kutembelea eneo la wanakijiji hao ambao wamekuwa "punching bag" la kujipimia nguvu wanajeshi !

Serekali ya kijiji na wanakijiji wa kimbiji wamebaki midomo wazi na kupatwa na mshangao
mkubwa kutokana na ukimnya wa serikali na vyombo vya dola kugeuka bubu kwa kutoingilia
kati sakata hili,wala kutotoa kalipio kali dhidi ya wanajeshi wenye tabia za kuwa nyanyasa
wanakijiji wa kimbiji na sehemu zingine ambazo zimeshafanyiwa vitendo vya kinyama na wanajeshi wa JWTZ

jaribu kuwasiliana na mwenyekiti wa kijiji kimbiji
simu 0713846688 hili kupata mkasa wenyewe ulivyokua

No comments:

Post a Comment