Friday, December 9, 2011


FFU wa NGOMA AFRICA BAND WAMESHATUA BERLIN!
Kwa kutumbuiza katika Sherehe za miaka 50 ya Uhuru
Ijumaa 9 na Jumamosi 10 Dec 2011 Berlin Hapatoshi FFU wa Ngoma Africa Band kutoa burudani ya kukata na Mundu, CD ya "50 Uhuru Anniversary" inatamba Redioni


Watanzania wanaoishi Ujerumani ! na Full Shangwe ya Miaka 50 ya Uhuru !

Berlin Chereko !Chereko ! Umoja wa Tanzania Ujerumani (UTU) kuzinduliwa rasmi ! 10-12-2011 Berlin!


Kikosi Kazi cha Ngoma Africa band aka FFU,kimeshatua mjini Berlin kwa kazi moja tu, nayo ni kushambulia na muziki wake katika kusherekea miaka 50 ya uhuru wa Tanzania.


Kuanzia 9 hadi 10-Dec-2011 mjini Berlin ambako ndipo hupo Ubalozi wa Tanzania na ndio mji mkuu wa Ujerumani,kutakuwa hapatoshi kwani sherehe hizo zitaambatana na ufunguzi wa UMOJA WA WATANZANIA UJERUMANI (UTU) siku ya jumamosi 10-12-2011,umoja huo unawaunganisha watanzania wote waishio ujerumani,ulitiliwa nguvu na balozi Mh.Ngemera, umeshasajiliwa na viongozi wake ni Bw.Mfundo Peter Mfundo(mwenyekiti) na Bi.Tullalumba Mloge (katibu),utaratibu unaonyesha kuwa sherehe hizo mjini Berlin zitaanza saa 9 mchana hadi usiku usio kwisha ambapo Ngoma Africa Band aka FFU,watatumbuiza na muziki wao,mahala patakapo fanyika sherehe Apostelkirche 1, 10738 Berlin,

UMOJA NI NGUVU WATANZANIA JITOKEZENI ! KUSHREKEA MIAKA 50 YA UHURU !

sikiliza muziki at www.ngoma-africa.com

No comments:

Post a Comment