Saturday, September 8, 2012

Harambee Ya Mjane Wa Daud Mwangosi Yavuka Malengo, Wengi Wanaendelea Kumchangia

1. Chris Cremence                                     100,000
2. Anonymous                                             500,000
3. Maggid Mjengwa                                     100,000
4. Raymond Kasoyaga                                   20,000
5.Edward Mgogo                                            10,000
6.Joachim Kiula                                                5,000
7.Libory Muhanga                                             5,000
8.Geofrey Kagaruki                                        10,000
9.Sadiki Mangesho                                         10,000
10. Edwin Namnauka                                      40,000
11.Daud Mbuba                                               10,000
 12. Anonymous                                             200,000
13.Mikidadi Waziri                                              6,000
14. Bungaya Mayo                                             5,500
15. Abraham Siyovelwa                                    50,000
16. Godfrey Chongolo                                       22,222
17. Jacob Mwamwene                                       51,000
18. Denis Bwimbo                                        153,683 
19. Zanzibar Ni Kwetu                                     150, 464
20.Felex Mpozemenya                                       10,000
21.Rweyendera Ngonge                                     11,000
22. Festo Temu                                                      10,000
23.  Azaria Mulinda                                                 10,000
24.Khatibu Kolofete                                                   5,000
25. John Bukuku                                                  25,000
26. Abel                                                                10,000
27. Hafidh Kido                                                     10,000
28. George Mtandika                                            16,000 
29. Shy-Rose Bhanji                                          200,000
30. Raymond Nkya                                               52,000
31. Maganga Sambo                                             10,000
32. Felix Mwakyembe                                             10,000
33. Abdul Diallo                                                         5,000
34.  Newton Kyando                                              20,000
 35. Galanos Myinga                                               20,000
36. Anonymous ( 200 Euro)                                    497,000   
37.   Yasinta Ngonyani                                              50,000
38.  Prosper/ Willy  ( Japan)                                    314,000
39.   Nuru Mkeremi                                                   131,000
40. Anonymous                                                            50,000
41.  Josephine Mahimbo                                              50,000
42.  Anonymous                                                         150,000
43. Heladius Macha                                                      30,000
44. Emma Malele                                                           10,000
45.  Anonymous                                                            60,000
46. Hendry Mlay                                                            35,000
47. Hosea Ngowi                                                            10,000
48. Athuman Zuber                                                           5,000
49. Hyancinth Komba                                                        7,500

                                            
Jumla:                                                   3,024,964   ( Milioni Tatu Na Ishir Na ini Na  Mia Tisa Na Sitini Na Nne)

 Lengo lilikuwa kukusanya 2,200,000 (Shilingi milioni mbili na laki mbili.) Hivyo, ndani ya saa 48 tumefanikiwa kufikisha na kuvuka lengo kwa shilingi 824,000 ( Laki nane na ishirini na nne elfu). Na michango zaidi bado inaendelea kutolewa. Mjengwablog itaendelea kupokea michango hiyo na kuikabidhi kwa mjane wa marehemu kama itakavyorekodiwa hapa. Hivyo, aliye dhamira ya kumsaidia mjane wa Marehemu bado anakaribishwa kutoa mchango wake. Siku ya mwisho ya kukusanya michango hiyo itakuwa Jumapili ijayo badala ya mwisho wa mwezi huu kama ilivyopangwa awali.)

Unaweza kuchangia kwa kutumia; M-Mpesa, Tigo Pesa, Airtel Money au NMB Mobile. Kwa namba 0754 678 252, 0712 95 61 31, 0788 111 765 ( Kwa walio nje mnaweza kutuma kwa Western Union, jina la mpokeaji- Maggid Mjengwa, Crdb A/ c 01j 2070759000 Maggid Mjengwa, NBC account ni 028201037642 jina Maggid Mjengwa. Tafashali nijulishe kama utatuma kwa njia ya Western Union au Benki)
Background:
Ndugu zangu, 
 Daud Mwangosi ambaye pia alikuwa ' Mwanakijiji' mwenzetu hapa  Mjengwablog hatunaye tena.
Nimemfahamu Daud Mwangosi  tangu mwaka 2004 nilipofika Iringa. Tangu wakati huo, amekuwa akiinipa ushirikiano mkubwa kwenye kazi ya kutangaza shughuli za kijamii kwenye  Vyuo Vya Maendeleo ya Wananchi. Ni  kwa kupiga picha za televisheni na kurusha habari kwenda Channel Ten; Iwe ni kwenda naye Ilula au Njombe, Daud Mwangosi  alikuwa tayari kila nilipomwomba aongozane nami kwa shughuli ya kijamii.

Mara nyingi nilimkuta Daud ofisini kwake  ( Picha ya kwanza juu) akichapa kazi na   huku mkewe akimsaidia kazi nyingine. Daud Mwangosi alikuwa mbunifu. Alikuwa ni mwenye kiu ya kujifunza mambo mapya kwenye teknolojia ya habari na mawasiliano.

Najua Daud Mwangosi alikuwa na  malengo ya kuendeleza shughuli zake za ujasiriamali.  Mbali ya mambo mengine, alikuwa na Photocopy machine ya kumwongezea kipato  ambayo iliharibika mwaka jana. Akawa na ndoto ya kuwa na studio ndogo ya kupiga picha za vipande ( Passport Size). Yote ni katika kumwongezea kipato kutunza familia yake.

Leo Daud Mwangosi hayuko nasi. Ameacha familia, mjane  na watoto wanne;  Itika Mwangosi ( Mjane) Nehemia Mwangosi ( 17) Kidato cha Nne Malangali Sekondari, Hetzgovina Mwangosi  (12) Bathsheba Mwangosi (9) na Moria Mwangosi ( 2)
Namini Daud Mwangosi angependa shughuli alizokuwa akizifanya ziendelee na zije kuwasaidia watoto wake pia.

Jana na leo nimewasiliana na mjane wa marehemu Mwangosi ambaye bado yuko Tukuyu. Nikamwambia kuna ' Wanakijiji ' wa Mjengwablog walioguswa na msiba wa Mwangosi na wangependa kutoa pole yao imsaidie katika kupata mwanzo kutoka hapa alipo sasa. Mjane wa Mwangosi amefarijika sana kusikia habari hizo. 

Kwa vile tayari ameahidiwa msaada wa kusomeshewa watoto. Msaada anaouhitaji kwa sasa ni kupata photocopy machine ( Used)  na kodi ya pango la ofisi. Jumla yake kwa yote hayo mawili haitazidi shilingi za Kitanzania milioni mbili na laki mbili. Hivyo msaada anaouomba kwa wenye mapenzi mema ni shilingi 2, 200,000 ( Shilingi milioni mbili na laki mbili). Shughuli hizo zitamsaidia kujikimu.

Kutokana na hali aliyo nayo sasa, Mwenyekiti wenu napendekeza nichukue jukumu la kuratibu michango hiyo.  Shime tushirikiane kufanikisha hili ili tumsitiri mjane wa mwenzetu Daud Mwangosi.
 Napendekeza ifikapo mwisho wa mwezi huu  ( Septemba) tuwe tumefanikisha zoezi hili kwa yeyote aliye nacho, hata kama ni shilingi elfu tano, ni msaada mkubwa.

Mjengwablog bado tuna rekodi nzuri katika kuchangishana kuwasaidia  wenye kuhitaji. Itakumbukwa, huko nyuma,  kwa pamoja, tulifanikisha kukusanya michango ile ya watoto wa Somalia na kuikabidhi UNICEF, Dar es Salaam. Ni zaidi ya shilingi milioni mbili.
Tulifanikisha mchango wa kusaidia ukarabati  wa maktaba ya Kijamii kijijini Mahango, Madibira. Zaidi ya shilingi milioni nne.
Sasa ni zamu ya kumchangia mjane wa mwenzetu Daud Mwangosi. Kinachohitajika ni milioni mbili na laki mbili.
Naam, kutoa ni moyo, usambe ni utajiri.
 Mwenyekiti wenu na familia yangu naanza kwa kuchangia shilingi laki moja.
Na kama kawaida, taarifa za waliochanga na kiasi kilichopatikana kitawekwa kwenye blogu kwa kila mmoja kuona.

Namna ya kuwasilisha michango: Tumia M-Mpesa, Tigo Pesa, Airtel Money au NMB Mobile. Kwa namba 0754 678 252, 0712 95 61 31, 0788 111 765 ( Kwa walio nje mnaweza kutuma kwa Western Union, jina la mpokeaji- Maggid Mjengwa)

Natanguliza Shukrani.

Maggid Mjengwa,
Iringa.
0788 111 765

No comments:

Post a Comment