Sunday, January 13, 2013

MAMIA WAMZIKA SHEIKH ABDALLAH M. JEMBE BAGAMOYO

Mamia ya waombolezaji wakibeba jeneza lenye mwili wa marehemu,Abdalla Masoud Jembe, aliyekuwa Sheikh Mkuu wa Bagamoyo, wakati walipowasili na jeneza hilo kwenye makaburi ya Mwanakarenge, mjini Bagamoyo kwa ajili ya maziko yaliyofanyika leo, katika Makaburi ya Mwanakarenge.
Sehemu ya waombolezaji wakiwa katika shughuli ya maziko ya aliyekuwa Sheikh Mkuu wa Bagamoyo, Abdalla Masoud Jembe, wa Bagamoyo.
Rais Jakaya, Makamu wake, Dkt Bilal, Mkuuwa mkoa wa Arusha, Magese, wakiwa katika shughuli za maziko ya aliyekuwa Sheikh, Mkuu wa Bagamoyo, Abdallah Jembe.
Rais Jakaya, akiweka mchanga katika kaburi la Abdallah, Jembe,wakati wa shughuli hiyo ya maziko iliyofanyika kwenye Uwanja wa Mwanakarenge.
Makamu wa Rais, Dkt. Bilal, akiweka mchanga katika kaburi la Abdallah, Jembe,wakati wa shughuli hiyo ya maziko iliyofanyika kwenye Uwanja wa Mwanakarenge.

Mbunge wa Bagamoyo, Shukuru Kawambwa, akiweka mchanga katika kaburi la Abdallah, Jembe,wakati wa shughuli hiyo ya maziko iliyofanyika kwenye Uwanja wa Mwanakarenge.



Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magese Mwilongo, akiweka mchanga.
Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Ahmed Kipozi, akiweka mchanga.
Mwenyekiti wa CUF, Ibrahim Lipumba, akiweka mchanga. 
Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM mkoa wa Pwani Ridhwani Kikwete, akiweka udongo katika kaburi la Shekhe Maarufu mjini Bagamoyo Shekhe Abdallah Masoud Jembe, wakati wa mazishi yaliyofanyika mjini Bagamoyo leo jioni. 
Waombolezaji wakiwania machepe kuweza kuweka mchanga katika kaburi hilo.

No comments:

Post a Comment