Tuesday, February 5, 2013

Je Wajua Kuwa Mazoea ni Sumu ya Penzi-Soma Hapa Ujue


Unaweza usijue mtu uliyenaye anakupenda kiasi gani kwa sababu ya mazoea,unachukulia Mapenzi yake,I love you zake,Chakula anachokupikia,Kukufulia nguo,na Zawadi anazokupa,kama mazoea...Ukawa busy kutompa haki yake na penzi analostahili kwa Penzi lake juu yako,ukawa bize na Kokoto zingine na kuiacha dhahabu yako nyumbani imejaa vumbi...Dhahabu hata ijae vumbi vipi haiwezi kuwa na thamani sawa na Kokoto ya Tegeta!Siku atakayoondoka utajikuta una lori zima la kokoto lakini halina thamani,utakuwa umepoteza Dhahabu ya thamani kwa sababu tu hukuijali ilivyopaswa na wengine waliotambua thamani yake waliijali on ur behalf!
Mapenzi hayana Mazoea,hata muwe na miaka H kwenye Mapenzi msiishi kama wazee,hakikisha Mapenzi yenu yananukia upya kama mmeanza jana,kila anayewaona awatamani...Mazoea yataua penzi lenu,Once ukiingiza Mazoea utaona dhabau ni kama bati wakati majirani wanaona jinsi inavyong'aa na wanaitamani...Respect your Lover,Value even the small things he/she does to you,hata akileta boxer ya 800 ya Karume mwambie asante maana atleast ulicross kwenye mind yake akanunua...Mazoea ni adui wa Mapenzi,Kill it!

No comments:

Post a Comment