Thursday, April 25, 2013

MAGIGE FOUNDATION YATOA MSAADA DODOMA


Mama Tunu Pinda akihutubia

Asasi ya Kijamii ya Catherine Foundation jana imetembelea kituo cha kulelea wa watoto cha Matumaini Village kilichopo mkoani Dodoma ambapo walikwenda kutoa misaada mbalimbali wakiongozwa na Mkurugenzi wa Asasi hiyo, Catherine Magige. 
Katika Hafla hiyo Mgeni Rasmi alikuwa Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda ambapo asasi hiyo ilitoa vitu mbalimbali vikiwemo, Madaftari, Mafuta, Sabuni, Juice, miswaki na dawa zake, mchele, sukari, nguo za watoto, kanga za wakinadada wanaowalea watoto hao na vingine vingi.
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda akihutubia katika hafla hiyo.
Mkurugenzi wa Catherine Foundation, Mhe Catherine Magige akihutubia katika hafla hiyo
Mkurugenzi wa Catherine Foundation, Catherine Magige akizungumza na watoto wanaolelewa kwenye Kito cha Matumaini Village kilichopo Dodoma alipokwenda kutoa msaada 
Mhe Catherine Magige akicheza na mmoja wa watoto wa kituo hicho
Mkurugenzi wa Catherine Foundation, Mhe Catherine Magige akiwa na mtoto mchanga anaye lelewa katika Kituo cha Matumaini Village mjini Dodoma jana.
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda na Mkurugenzi wa Catherine Foundation, Mhe Catherine Magige wakizungumza na watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho.
Mama Tunu Pinda na Mhe Catherine Magige wakiwa na watoto hao
Mama Tunu Pinda akikabidhi zawadi mbalimbali zilizotolewa na asasi hiyo 
Misaada mbalimbali ikitolewa
Mkurugenzi wa Catherine Foundation, Catherine Magige akizungumza na watoto wanaolelewa kwenye Kito cha Matumaini Village kilichopo Dodoma alipokwenda kutoa msaada

No comments:

Post a Comment