Thursday, October 31, 2013

Q-CHILA "NIMEOTESHWA NDOTO YA USHINDI KUWA PAPII KOCHA ATARUDI URAIANI"

Muimbaji wa Beautiful, Q-Chilla amesema ameota ndoto kuwa Papii Kocha na baba yake Nguza Viking aka Babu Seya wataachiwa huru.

Leo, Jumatano, jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani nchini Tanzania limeipitia upya hukumu yao.

“Nimeota ndoto ya ushindi, nimemuona Papii Kocha Sinza anakatiza barabara. Naotaga mara chache sana na huwa vitu vinatokea. Iko wazi kaka yangu anarudi uraiani. Nimemuona, welcome home, dunia ilikumiss, vita imekwisha,” Q-Chilla ameimbia Bongo5.

“Let the world know that the beloved kid is coming home.”

Katika rufaa hiyo leo wakili wa Babu Seya na Papii Kocha ameiomba mahakama hiyo ifute ushahidi na waachiwe huru lakini serikali imepinga. Kutokana na hatua hiyo, leo mahakama ya rufaa haijafanya uamuzi wowote imewapiga kalenda.

Nguza Viking na Papii Kocha wanatumikia kifungo cha maisha jela kwa makosa ya kubaka na kulawiti watoto wadogo wa shule ya msingi.

No comments:

Post a Comment