Saturday, July 31, 2010



Kida Waziri arudi tena uwanjani!

Ni mmoja ya wanamziki wanawake wachache sana ! ambao wamezaliwa na vipaji mwanadada Kida Waziri,  maarufu kama "Stone Lady" ambaye ana sauti ya kumtoa nyoka pangoni!.

Mwanamziki Kida Waziri ni mjukuu wa Mshairi maarufu barani Afrika marehem Shaban Robert, pia ni mtoto wa aliyekuwa mwanadiplomasia miaka ya 70s na 80s balozi Bw.Waziri Juma.

Habari za uhakika zinasema kuwa Dada Kida Waziri karudi umpya katika ulimwengu wa mziki baada ya kumpumzika kwa miaka,Mwanamziki Kida Waziri "Stone Lady" ambae amerudi na Album ya nyimbo 6,ambayo inamziki uliojaa mdundo na sauti ambayo ni almasi tupu.....

Labda ungependa kuwa moja ya wadhamini ,au Kufanya Kazi na mwanamziki huyo Kida "Stone Lady" Waziri.

Mwanadada huyo yupo tayari kupiga Tour ya ndani na nje ya Tanzania anapatikana kwa simu namba 0754697114 ukipiga nje ya Bongo Tel. + 255(0)754697114

No comments:

Post a Comment