Saturday, September 24, 2011

Upi ? Msimamo wa viongozi wa nchi Afrika kuhusu Libya?
Je ? wanamtambua kiongozi halali wa Libya?
Vipi ? kiongozi wa waasi Mustafa Abdel-Jalil anatambulika na Viongozi wetu?
 

Wakati viongozi wa nchi mbali mbali wamekutanika mjini New York, kwa ajili ya mkutano wa umoja wa mataifa UN, katika mkusanyiko huo wamo pia viongozi wetu kutoka nchi za kiafrika ambao pia ni wanachama wa umoja wa Afrika AU, ambayo Libya pia ni mwanachama wa AU,lakini utata unakuja nani kiongozi halali wa nchi hiyo Libya? Kanal Gaddaf au Mstafa Abdel-Jalil ambaye nae yupo huko New York.
 
Swali lingine kubwa ambalo wengi wetu tunajiuliza je ?viongozi wa nchi za  Afrika wanautambua uhalali wa Mstafa Abdel- Jalil ?kama hawautambui je? watakubali kuwepo ukumbini na kumsikiliza otuba ya kiongozi huyo aleyeingia  madarakani kwa njia ya bunduki tena kwa kusaidiwa na NATO? au watakuwepo
ukumbini kwa mithali za kiswahili kila moja na lwake? yaani ya Ngoswe muachie Ngoswe! je? fadhila za Kanal Gaddaf na mchango wake katika bara la Afrika  ndio zitakua zimesauliwa.
 
Mengi tunajiuliza lakini siye wafrika tunategea sikio uko UN kusikiliza msimamo wa viongozi wetu juu ya kauli ya pamoja kuhusu maslahi ya bara la Afrika.

No comments:

Post a Comment