Saturday, September 24, 2011

ANGALIZO ALILOLITOA WAZIRI MKUU MSTAAFU CLEOPA D. MSUYA KUHUSU HALI YA UMEME NCHINI LIZINGATIWE.

Mh. Cleopa David Msuya.
Athari ambazo zinaweza kutokea kutokana na Taifa kuendelea kuwa kizani, wananchi wanaotegemea nishati hii kama nyenzo yao ya kujipatia kipato na uhitaji wa Nishati hiyo Mahospitalini, inaweza kutupeleka Watanzania tukaingia kwenye vugu vugu la wananchi kutaka kuitoa Serikali iliyo madarakani kwa njia maarufu inayoitwa 'NGUVU YA UMMA' kama mataifa mengi ya Kiislam yalivyotokea; mfano hai ni Misri.

Hayo yalisemwa na Mh. Msuya wakati alipokua kwenye mjadala wa kitaifa kuhusu miundombinu, nishati na madini katika Wiki ya Maonyesho ya Miaka 50 ya Uhuru yaliyoandaliwa na Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF).

No comments:

Post a Comment