Saturday, April 21, 2012

Taswira Za Yale Maandamano Ya Wanaharakati Wanaodai Kura ya Maoni Dhidi ya Muungano Zanzibar .

Jeshi la Polisi likitoa tahadhari kwa wananchi waliofika katika viwanja vya baraza la wawakilishi wakidai kuwepo kwa kura ya maoni juu ya Muungano
Mdau wa kikundi cha Wazanzibari wanaodai kuitishwa kura ya maoni dhidi ya Muunganoakisindikizwa na polisi kuondoka sehemu ya maandamano

Kiongozi wa kikundi cha Wazanzibari wanaodai kuitishwa kura ya maoni dhidi ya Muungano Rashid Salum Adiy akizungumza muda mfupi baada ya kushikwa na polisi kwa kufanya maandamano kinyume na sheria

Kikosi maalum cha Polisi cha kuzuia fujo kikijipanga kukabiliana na wanaharakati waliofika baraza la Wawakilishi jana

Hashim na wenzake wakiwa katika gari la Jeshi la Polisi likiwachukua na kuwapeleka Madema, baada ya kukusanyika katika viwanja vya baraza la wawakilishi wakidai kuwepo kwa kura ya maoni itakayoamua kuwepo au kutokuwepo Muungan.Picha na Habari na Mdau Othman Maulid

No comments:

Post a Comment