Monday, January 7, 2013

JK IGUNGA KUKAGUA MAENDELEO


Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na wakazi wa Igunga.
Rais Jakaay Mrisho Kikwete akihutumia mamia ya wananchi wa Igunga katika mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika uwanja wa Barafu mjini Igunga baada ya kuzindua ujenzi wa daraja la Ndutu pamoja na mradi mkubwa wa maji utaohudumia asilimia 70 ya wakazi wa Igunga.
Maelfu ya wakazi wa Igunga wakimsikiliza Rais Kikwete
Rais Kikwete akikata utepe kama ishara ya uzinduzi wa ujenzi wa Daraja.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua mradi wa Chujio la maji safi kwa mji wa Igunga sehemu za Bulenya ambapo wakazi asilimia 70 wa mji huo watapata maji safi
Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli akijiunga na bendi ya Msondo Ngoma kutumbuiza wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa daraja la Mbutu la Igunga


Wananchi wakivuka katika sehemu itayojengwa darala la kisasa la Mbutu la Igunga ambao ujenzi wake umezinduliwa leo na Rais Jakaya Mrisho Kikwete, hatua ambayo itatatua kabisa tatizo la miundombinu.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na kutoa ushauri kwa kundi la vijana 10 ambao baada ya kumaliza chuo kikuu wamejikusanya na kuunda kikundi cha ujasiriamali mjini Igunga wakijishugulisha na Kilimo
Rais Kikwete akiangalia michoro ya Daraja litakalojengwa.

No comments:

Post a Comment