Tuesday, October 22, 2013

CATHERINE FOUNDATION YAZINDULIWA RASMI JIJINI ARUSHA

Mwemyekiti wa Taasisi ya Catherine Foundation ambaye pia ni Mbunge wa viti Maalum UVCCM Arusha, Catherine Magige akizungumza wakati wa uzinduzi wa taasisi yake uliofanyika hivi karibuni jijini Arusha.


Catherine Foundation ni taasisi isyofungamana na upande wowote na inatoa huduma za kijamii kwa makundi mbalimbali yakiwapo ya Vijana, watoto na wanawake wajane
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angela Kairuki akizungumza wakati akizundua rasmi taasisi ya Catherine Foundation.
Mbali na uzinduzi huo Catherine Foundation ilitoa msaada wa vitu mbalimbali kwa watu wenye uhitaji maalum.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angela Kairuki (kushoo) akizndua rasmi ofisi za taaisi ya ‘catherine Foundation’ iliyo jijini Arusha, katika uzinduzio uliofanyika mwishoni mwa wiki jijini humo. Pamoja nae ni Mwenyekiti wa Taasisi hiyo ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum UVCCM-Arusha,Catherine Magige.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angela Kairuki akifurahia mandhari nzuri ya ofisi ya Catherine Foundation. Kulia ni Mwenyekiti wa taasisi hiyo na Mbunge wa viti Maalum Arusha, Catherine Magige.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angela Kairuki akitia saini kitabu cha wageni.
Mwenyekiti wa taasisi hiyo na Mbunge wa viti Maalum Arusha, Catherine Magige akiwa na watoto mbalimbali.
Hapa ndo ilipo Ofisi za Catherine Foundation. Ni Katika barabara ya Moshi Arusha, PPF Kaloleni mtaa wa Makanyaga katika nyumba za Denafro ghotofa ya 1.

No comments:

Post a Comment